DANIEL SURA YA SABA SEHEMU YA PILI.

FALME ZITAKAZOWAATHIRI WATU WA MUNGU

(SEHEMU   YA   PILI)

(SOMA DANIELI 7:7-14,18,20-28)

Karibu tena rafiki tunapoendelea na unabii wa kitabu cha Daniel somo la nyuma linatupa ufunguo tunapoendelea na hii sehemu ya pili kumbuka Katika  Sehemu  hii  ya  Pili  tuna  kazi  moja  tu  ya  kufanya;    kuthibitisha  kwamba "Pembe Ndogo" inawakilisha Ufalme wa Papa au Upapa kama baadhi ya ndugu wamejaribu kuuliza hivi hii pembe ni kitu gani? wengine wakauliza alama au chapa ya mnyama ni IPI ninakutoa shaka Mpendwa haya yote kila mtu anatamani kuyaelewa vyema utayaelewa endelea kufuatilia masomo haya ,hata sura hii imegusia hayo maswali , pia sura ya nane imeweka wazi pia katika hilo .ilituweze kuitambua vyema hii pembe ndogo lazima tuangalie sifa zake , unajua watu iliwaweze kumkamata wachawi wana vigezo  vyao vinavyothibitisha kuwa  huyo  kweli  ni mchawi.    
Mungu  naye ameweka vigezo vyake ili  kumtambulisha "Pembe  Ndogo"  na  kuondoa  mashaka  yo  yote waliyo  nayo  watu kuhusu  suala  hilo.   Tutatumia  mafungu  ya  Biblia  huku  na  huku  (Isa.  28:10)  pamoja  na Ushahidi wa  Historia.  
 Kwa nini  tusumbuke  kuutambua  ufalme huo?  
Kwa  sababu  ufalme huo utasababisha wanadamu wote duniani  watakaoambatana  nao  kuangamizwa  pamoja nao (Ufu.19:11-21).
Kama nilivyosema huko nyuma, ufalme  huu  una  majina  mengi  katika  kitabu  cha Danieli  na kile  cha Ufunuo.  
Tutajaribu kujenga  daraja  la kuunganisha Danieli  7  na  Ufunuo 13  kwa  kuangalia  vigezo  vichache  tu  miongoni  mwa  vingi.   Hukumu  iliyotajwa  katika Danieli 7 imeamua  kumwondolea  ufalme  na  kumwangamiza,  lakini  baada  ya  kupewa utawala wake wa Awamu ya Mwisho (Dan. 7:26;   Ufu. 19:1-3;  18:4-8;  16:1,2,10,19-21;  17:1-11).   Hebu na tuziangalie hizi Sifa za pembe ndogo iliyozuka kati ya zile kumi na kuziondoa tatu .

 KIGEZO  1:    PEMBE  NDOGO  ILIKUJA  BAADA  YA  FALME  10  KUJITAWALA (Dan.7:8)

 Falme 10 za Ulaya Magharibi zilizotajwa katika Sehemu ya  Kwanza  ya  somo  hili zilijitawala mwaka 476 B.K. mara tu baada ya Ufalme wa  Warumi  kuangushwa.  
 Baada ya  kuanguka  ufalme huo  Askofu wa Rumi,  ambaye  baadaye aliitwa  Askofu  wa Maaskofu au  Papa,  alitawala  katika  mji  wa  Roma  tu  mpaka  mwaka  538  B.K.  alipoitawala  Ulaya Magharibi.  Historia inaunga mkono.

KIGEZO 2:   PEMBE NDOGO   ILIZING'OA PEMBE TATU KABLA YA KUTAWALA

Falme  tatu  zilizong'olewa  kwa  amri  ya  Papa  (Dan.  7:8,20,24)  ni  hizi  -   Waheruli waling'olewa mwaka 493 B.K.;  
Wavandali (Vandals)  waling'olewa  mwaka  534  B.K.;
  Waostrogothi (Ostrogoths)  waling'olewa  mapema  mwaka  538 B.K.  
Kwanini haya mataifa yaling'olewa na huu ufalme.?
Mataifa  hayo  matatu yalikuwa yanampinga  Papa.    

Yale  mengine  7  kufikia  mwaka  508  B.K.  yalikubali  kuwa wakatoliki  kwa kulazimishwa  na  mfalme wa  Ufaransa,  Clovis, mwana  mpendwa  wa Papa.  Historia inathibitisha.

KIGEZO 3: PEMBE NDOGO ILIKUWA TOFAUTI NA  PEMBE  ZILE  KUMI  (Dan. 7:24).    

Je utofauti wake ukoje ? 

 Pembe 10 ni falme za kisiasa za Ulaya Magharibi.

 Pembe Ndogo ni Ufalme wa  Papa wa Kidini-Kisiasa.   Historia inaunga  mkono.  
 Kanisa  la  Kikristo ulimwenguni halina  utawala wa kisiasa (Yoh. 18:33-38).  Kwa hiyo, Ufalme wa Papa umepata mamlaka  yake  kutoka kwingine,  si  kwa  Mungu ,soma mafungu haya rafiki . (Ufu.  13:1,2;    12:9).    Hii  ndiyo  maana  wanaouunga  mkono wataangamizwa pamoja nao.
 Serikali  zote  za  kisiasa za dunia  zimepewa mamlaka  yao  na Mungu (Rum. 13:1-7;  1 Tim. 2:1-6).  Kwa ajili hiyo zinawaadhibu wahalifu  na  kuwasifu raia wema.   Ufalme wa Papa  unawaua watu  wema (watakatifu)  na  kuwaacha hai  wahalifu soma rafiki hapa (Dan. 7:21)

KIGEZO 4:  PEMBE NDOGO ILITAWALA KWA MIAKA 1260

Ninaomba rafiki hapa twende taratibu ilituelewane soma  (Dan. 7:25). Katika biblia Wakati  mmoja   ni  sawa  na  mwaka mmoja.  

  Kwa  hiyo  wakati  1  +  2  +  1/2  =  Nyakati 3 1/2 = Miaka 3 1/2.  

 Mwaka 1 una miezi 12.  
 Kwa hiyo, miaka 3 1/2  = Miezi 3 1/2 x 12 = Miezi 42.  Mwezi wa Biblia una siku 30 (Dan. 6:7;  Mwa. 7:24).  Kwa hiyo miezi 42 = siku  42  x  30  =  siku  1260.   Siku  1 ya unabii  =  mwaka  1  wa  kawaida.   Hivyo siku  1260 ni miaka ya kawaida  1260.  

 Angalia  maajabu!   Mnyama yule  wa Ufunuo  13:1-10,18  alipewa kufanya  kazi  yake  kwa miezi  ile  ile  42 (Ufu.  13:5).   Ajabu  zaidi  ni  kwamba  Joka  lile  Kubwa Jekundu la Ufunuo 12 linawakilisha  Rumi  ya  Kipagani  iliyotaka  kumwua  Kristo  kupitia kwa Herode (Ufu.12:2-5;   Mt. 2:16) na tena linaiwakilisha  Rumi ya  Kipapa (Ufu. 12:6,14) ambapo  tunaona  mwanamke (kanisa la  Mungu  la kweli)  akikimbilia nyikani  kwa  siku  1260 au miaka 1260.  Kigezo hiki kinajenga daraja ya  kuitambua  Pembe  Ndogo  ya  Danieli  7 kuwa  ni  Mnyama  yule  kama  Chui  wa  Ufunuo  13.   Tabia  zinalandana  sana.  
 Upapa ulitawala kihistoria kuanzia 538 hadi 1798 B.K., miaka 1260 kamili.

KIGEZO 5:  PEMBE NDOGO ILIWAUA WATAKATIFU (Dan. 7:21,25).

Zaidi  ya watatifu  milioni  50  waliuawa  katika  kipindi  cha  utawala  wa  papa  cha  miaka 1260  kwa  kosa  la  kufuata  mafundisho  ya  Biblia.   Aliwaita  "wazushi"  (heretics);   Biblia inawaita "watakatifu".  Ni kweli upapa ulikuwa umelewa kwa  damu  ya  watakatifu  (Ufu. 17:6).  
Ni jambo la kushangaza mno kwa kanisa kuua  kanisa!    Linganisha  na  Ufu.  13:7.  Ni ufalme ule ule mmoja.

KIGEZO  6:   PEMBE  NDOGO  ILIAZIMU  KUBADILI  MAJIRA  NA  SHERIA  (Dan. 7:25).

Sheria  ni  Amri  Kumi  za  Mungu  (Kut.  20:3-17).   Upapa uliazimu kuifuta  kabisa Amri ya Pili inayokataza ibada ya sanamu.  Angalia Katekisimu  za  Kanisa  Katoliki  pamoja  na Misale utashangaa.   Amri ya Nne inayohusu  Sabato akaibadili  na  kuweka  Jumapili badala yake.
 Kwa hiyo ibada ya Jumapili iliwekwa na Papa kinyume cha Amri ya Nne.  Katika kitabu cha Ufunuo Jumapili  inaitwa  "chapa"  au  "alama"  ya  Mnyama,    yaani,  Alama  ya Mfalme Papa (Ufu.  13:l6,17).  

Katika  gazeti la  The Catholic  Record, London,  Ontario, la Septemba 1, 1923 maneno haya yamenukuliwa:

 "Jumapili ni alama yetu  ya  mamlaka....  Kanisa li juu ya Biblia,  na uhamishaji huo wa  utunzaji wa Sabato [Jumamosi]  ni ushahidi wa ukweli  huo."    Sasa  zikawa  zimebaki Amri 9,  sio  10.  Akaigawa Amri  ya  10  katika  amri mbili kufidia ya pili iliyofutwa kabisa.

 KIGEZO  7:   PEMBE  NDOGO  INANENA  MANENO  MAKUU  YA  MAKUFURU (Dan.7:8,20)

Hapa tutaangalia makufuru  mawili tu.

  Kufuru  la kwanza  ni madai  ya  kuwa  yeye ni Mungu  (Yoh.  10:30-33).  

Kwa  vipi?    Nanukuu:    "Papa  ana  cheo  kikubwa  mno,  tena ametukuzwa mno kiasi  kwamba yeye si mwanadamu tu, bali kama ilivyo  ni Mungu, tena ndiye aliye Badala ya Mungu."  
-----    Lucius  Ferraris,  Prompta  Bibliotheca  Canonica, Gombo la VI, uk. 438,442, chini ya makala "Papa".   Cheo cha Mungu alichojinyakulia ni "Baba Mtakatifu" (Yoh. 17:11).

 Kufuru la pili ni kudai kuwa anao  uwezo  wa  kusamehe dhambi

jukumu ambalo ni la Mungu  peke  yake  (Luka  5:20,21).  
Mungu  peke yake ndiye anayeabudiwa (Mt. 4:10);  lakini papa anataka  aabudiwe (2 The. 2:3,4;  Ufu. 13:4,7,8,12).  Linganisha na Ufu. 13:1,5,6.  
Ni mamlaka moja ile ile.
Mungu  hataki  watu  wake  wawe  gizani  kuhusu  ufalme  huu,  japo  kwa  sasa ulimwengu  unauinua  juu  sana.    Hatimaye  utakapotawala  kama  alivyoruhusu  Mungu itakuwa kwa  maangamizi  ya  ulimwengu  mzima  na dunia  itafikia  mwisho  wake (Ufu.  17:811; 6:14-17; 19:11-21).   Usiwe miongoni mwa wale wanaofanya mambo kwa kupelekwa bila kujua ashukuriwe Mungu maana amekuonesha baadhi ya siri juu ya hii pembe ndogo .kumbuka mwisho wa haya yote kutakuwa na makundi mawili ,wale wanaokubali kuteswa kimwili kwaajili ya ukweli ,na wale watakaopoteza hata nafsi zao kwa mauti ya milele,tutaendelea na sura ya saba lakini kumbuka kwamba wale watakaosimama katika kweli yote wakipingana kwa imani dhidi ya hii pembe  watakwenda  mbinguni  kutawala pamoja  na Yesu kwa miaka 1000 (l The. 4:16,17(18);  Ufu. 20:4).  Dunia hii itakuwa  imeharibika vibaya kipindi chote cha miaka  1000  (Yer.  4:23-27).    Baada  ya  kwisha  miaka  1000  watakatifu watarudi  hapa  pamoja  na  Mji  Yerusalemu  Mpya  (Ufu.  21:10).  
Ndipo  waovu watakapofufuliwa na kujaribu kuuteka Mji Yerusalemu Mpya  au  Kambi  ya  Watakatifu. Moto utawala (Ufu. 20:7-10,15). Hiyo ndiyo Jehanum au Ziwa la Moto  au  Mauti  ya  Pili (Ufu.  20:14).   Jehanum  haiwaki  sasa.   Itawaka  baada  ya  miaka  ile  1000  kwisha. Watakaoingia humo watateketezwa na kuwa majivu pamoja na Shetani na malaika zake( Mal. 4:1-3;   Eze. 28:14-19).  
Hawatafufuliwa tena milele!   Ndipo  watakatifu watakapoirithi nchi mpya (Ufu. 21:1; Mt. 5:5; 2 Pet. 3:10-13;  Zab. 37 yote).
NInaomba tuwe miongoni mwa watakatifu wanaosimama katika maandiko nasio mapokeo hawa wanajurikana ,wao biblia na biblia pekee ndio msingi wao na ndio wanaoendelea kukuletea habari njema zisizofundishwa mahali popote pengine ,ninakuarika Mpendwa endelea kufuatilia masomo haya ,Fanya tafakari moyo ni mwako ,omba Mungu akufungue zaidi ,nnaamini katika Kristo atakubariki .

Karibu kwa somo linalofuata sura ya nane.
Previous
Next Post »