PEMBE NDOGO YA DANIELI 8
(SOMA DANIELI 8 YOTE)
Ninapenda kuwakaribisha katika muendelezo wakujifunza neno la Mungu hasa katika unabii wa Daniel, kwanza ninapenda kuweka wazi jambo hili ,hatufundishi kwa kushambulia dhehebu au dini bali tunasema yaliyo kweli hasa ,kwahiyo usidhani kuna mabishano ya hoja ,hapana tunasema na kweka huru ukweli ili mtu mwenyewe asome ,alinganishe na kufanya uamuzi yeye mwenyewe ,jambo jingine ni kwamba MUNGU huwa anawapa taarifa watu wake kabla ya maafa kuwapata ,kwahiyo haya ni maonyo kwa watu wake kuhusu yale ambayo yanaendelea iliyatakapo tokea asiwepo mtu atakayesema Mimi sikuyasikia ,wala sikuambiwa ili hukumu itakapokuja kila mtu aseme HAKIKA HUKUMU ZAKO NI ZA HAKI NAZA KWELI .
Kwahiyo hatutoi mafundisho kwa kujaribu tunatoa ukweli kama ulivyo ,ni kweli unapoguswa lazima utafute njia ya kujitetea lakini kumbuka wokovu ni maamuzi yako ,muda Utakuja ambapo neno la Mungu halitaonekana tena ,ninacho kushauri usichoke kujifunza neno la Mungu omba Mungu akufunulie zaidi ,utabarikiwa na uzima wa milele uaambatana nawe.
Kumbuka kama tulivyoona kuwa Pembe Ndogo ya Danieli 7 inawakilisha Ufalme wa Papa. Lakini Pembe Ndogo ya Danieli 8 inaziwakilisha falme mbili ----- Rumi ya Kipagani na Rumi ya Kipapa.
Ni sawa tu na lile Joka Kubwa Jekundu la Ufunuo 12 lenye vichwa saba na pembe kumi ambalo linaziwakilisha falme zizo hizo mbili. Utazitofautisha kwa vitendo vyake tu.
Mungu haoni tofauti yo yote kati ya Rumi ya Kipagani na Rumi ya Kipapa.
Yesu aliziita falme zote mbili "Chukizo la Uharibifu," yaani, Mamlaka Zinazowaangamiza watu wa Mungu (Mt. 24:15,22; Dan. 9:27). Danieli 8 na 9 ni kitu kimoja; Gabrieli alishindwa kuendelea kumweleza Danieli habari za Pembe hiyo Ndogo ambayo itawaua watakatifu kiasi cha kustaajabisha kwa vile alikuwa amezimia (Dan. 8:24,27).
Baada ya muda kupita Gabrieli alimjia tena Danieli akamwambia anataka kumpa ufahamu wa njozi ya Danieli 8 ambayo alikatisha kumweleza (Dan. 9:20-22). Lakini kwa urahisi wa kuelewa tutachukua kila sura peke yake. Katika sura ya 8 kuna maono ya aina mbili ----- Kondoo mume mwenye pembe mbili (Dan. 8:3,4) ambaye anawakilisha Ufalme wa Wamedi na Waajemi (Dan. 8:20); kisha akaona Beberu mwenye pembe mashuhuri kati ya macho yake (Dan. 8:5-8) ambaye anauwakilisha Ufalme wa Wayunani (Dan. 8:21). Ile pembe mashuhuri ni mtawala wa kwanza Iksanda Mkuu (Dan. 8:21). Zile pembe nne ni majemadari wake wanne waliotawala baada ya kufa kwake Iskanda Mkuu (Dan. 8:22). Cassander alitwaa Jimbo la Magharibi; Lysimachus Jimbo la Kaskazini; Seleucus Jimbo la Mashariki (Siria kwenda mashariki), Ptolemy Jimbo la Kusimi (Misri na visiwa).
Falme hizo za Kiyunani zilipigana zenyewe kwa zenyewe; hatimaye Seleucus akachukua eneo lote la mashariki, kaskazini, na magharibi baada ya kuwashinda wenzake.
Ni katika pembe (ufalme) ya Seleucus ilimotokea Pembe ile Ndogo ambayo inaiwakilisha Rumi ya Kipagani, na hatimaye Rumi ya Kipapa (Dan. 8:9). Kwa maneno mengine Ufalme wa Warumi ulitokea katika eneo la Seleucus alilotawala.
Hiyo ni kweli kijiografia na kihistoria. Sasa tutaangalia mambo machache tu juu ya kazi iliyofanywa na Pembe hiyo Ndogo ya Danieli 8. Mungu kwa mkono wa Musa alikuwa amewaonya Waisraeli kuwa atawaletea taifa ambalo lugha yake hawaijui, litawazingira, watakula watoto wao; hayo yalitokea mwaka wa 70 B.K.
majeshi ya Warumi yalipouzingira Yerusalemu na kuuharibu kabisa pamoja na hekalu lake (Kum. 28:49-57; Dan. 9:26,27; Mt. 24:15-20; Luka 21:20-24). Ukatili wa falme hizo zinazowakilishwa na "mfalme mwenye uso mkali", yaani, katili, umedokezwa (Dan. 8:23,24). Wayahudi walijua Kiyunani lakini sio Kilatini. Agano jipya liliandikwa kwa Kiyunani, lugha ya Dola ya Wayunani.
Falme zote mbili, Rumi ya Kipagani na Rumi ya Kipapa zilitumia hila katika kutawala kwao (Dan. 8:25). Soma Historia ya Kale. Mpaka hapo ni mambo ya jumla. Sasa na tuangalie vitendo vya falme hizo kwa uchache tu:
RUMI YA KIPAGANI:
Pembe Ndogo ilikua sana kuelekea nchi ya uzuri, yaani, Palestina (Dan. 8:9). Palestina ilichukuliwa na kuwa sehemu ya Rumi ya Kipagani mwaka 63 K.K. "Jeshi la mbinguni" ni watu wa Mungu, "nyota" ni viongozi wa dini (Dan. 8:10: Ufu. 1:20). "Kuangusha chini na kukanyaga" ni kuangamiza au kuua. Ufalme huu ulitimiza hayo mwaka 70 B.K. ulipouangamiza Mji wa Yerusalemu, kisha katika karne ya pili uliua wakristo wengi chini ya Kaisari Diocletian wa Rumi.
Hata kabla yake wakati wa Nero mauaji ya Wakristo yalifanyika. Historia inaweka idadi ya waliouawa na Rumi ya Kipagani takriban milioni 3. "Patakatifu pakaangushwa chini" ni kuliharibu hekalu mwaka 70 B.K. (Dan. 8:11). "Mkuu wa Jeshi" au "Mkuu wa wakuu" ni Kristo mwenyewe (Dan. 12:1. Ufu. 12:7,8; Yoshua 5:13-15; Ufu. 1:5). Neno "malaika" maana yake "mjumbe". Linaweza kutumika kwa Kristo na kwa viumbe wale wa mbinguni tunaowaita malaika (Ebr. 1:14), au kwa "wachungaji" (Ufu. 2:1,8,12,18; 3:1,7). "Mikaeli" ni jina la Yesu anapokuwa Mkuu wa Majeshi ya Malaika (Amiri Jeshi wa Jeshi la Bwana).
Sauti yake ndiyo itakayowafufua wafu (Yoh. 5:25,28,29; 1 The. 4:16), anaitwa Malaika Mkuu. Huyo Pilato, Gavana wa Rumi ya Kipagani, alikabiliana naye ana kwa ana kama ilivyotabiriwa katika Dan. 8:11,25 (Yoh. 18:33-37; 19:1-3,10,11,23,19-22). Alisulibiwa juu ya msalaba wa Kirumi; alipigwa kwa mijeledi ya Kirumi, na kupigiliwa kwa misumari ya Kirumi, na kaburi lake likalindwa na askari wa Kirumi. Unabii huo ulitimia mia kwa mia.
RUMI YA KIPAPA:
Tutaangalia mambo kadhaa tu, sio yote. Rumi ya Kipapa ili"iangusha kweli hata chini" (Dan. 8:12). Kweli ni nini? Kweli ni Neno la Mungu, kweli ni Sheria ya Mungu (Amri Kumi). Soma Yoh. 17:17; Zab. 119:142. Upapa umeikanyaga chini ya miguu yake Sheria ya Amri Kumi kwa kufuta Amri ya pili inayokataza ibada ya sanamu, na kuweka Jumapili badala ya Sabato (Jumamosi) kama siku ya ibada (Dan. 7:25; Ufu. 13:16,17). Jumapili katika unabii inaitwa "Chapa au Alama ya Mnyama", yaani, Alama ya Uwezo wa Mamlaka ya Papa.
Sabato inaitwa Muhuri wa Mungu (Ufu. 7:1-4) au "Alama ya Mungu" (Eze. 9:4-11).
Martin Luther aligundua makosa (mafundisho potofu) 95. Sasa ni zaidi kuliko hayo. "Kukanyagisha patakatifu na jeshi"; yeye hajaliangusha jengo la hekalu, ila amegeuza mawazo ya waumini kumwelekea yeye badala ya Kuhani Mkuu, Yesu Kristo, katika Hekalu la Mbinguni kwa kuanzisha ukuhani na misa (Ebr. 4:14-16; 3:1). Kosa lingine ni lile la kutumia cheo cha Mungu cha "Baba Mtakatifu" (Yoh. 17:11). Muda hautoshi kuorodhesha mafundisho potofu yanayoitwa "mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake" (Ufu. 14:8; 17:2). Unafundisha Mapokeo badala ya Biblia (Mt. 15:3-9; Marko 7:5-13). Uliua watakatifu zaidi ya milioni 50 katika kipindi chake cha utawala wa miaka 1260 (538-1798), kiitwacho Zama za Giza (Dan. 8:24,25; Mt. 24:21,22). Waliomo katika mfumo huo wa utawala wanaambiwa watoke (Ufu. 18:4,5). Maana yake watoke katika kuabudu bila kufuata maagizo ya Mungu namna ambayo wanasema kuabudu ,hapa watu wote kuanzia anayekalia kiti cha papa hadi mlei wanatakiwa watoke katika huo mfumo maana mungu mwenyewe wanasema watoke .Na mamilioni watatoka kwa dhiki kubwa pamoja na kuuawa na wale watakaobaki katika mfumo huo (Ufu. 15:2; 20:4). Katika Danieli 7:9,10 hukumu ilifuatia baada ya upapa kufanya kazi yake kwa miaka 1260. Hapa pia tunaona hukumu ile ile ikirudiwa kwa maneno haya: "Hata nyakati za jioni na asubuhi elfu mbili na mia tatu; ndipo patakatifu patakapotakaswa" (Dan. 8:14). hili somo nitalitolea Maelezo baada ya hili kuisha ,na somo la patakatifu litafuaata. Mpango wote wa wokovu umedhihirishwa katika Hekalu la duniani na lile la Mbinguni (Ebr. 8:1,2; 9:6,7; Law. 16 yote; Law. 23:27-32). Tangu Sinai hadi Yesu alipokata roho msalabani huduma hiyo iliendeshwa na makuhani pamoja na kuhani mkuu na kufikia mwisho wake (Kut. 25:8; Mt. 27:50,51).
Yesu alipopaa mwaka 31 B.K. alikwenda moja kwa moja katika huduma ya chumba cha kwanza cha Hekalu la mbinguni (Ebr. 9:11,12) kama Kuhani Mkuu.
Siku 2300 za Dan. 8:14 ni siku za unabii, ni sawa na miaka 2300 (Eze. 4:6). Zilianza kuhesabiwa wakati ule amri ya kuujenga upya Yerusalemu ilipotolewa mwaka 457 K.K. na kukoma 1844 B.K. Kutakaswa kwa Patakatifu ni kazi ya Hukumu au Utakaso au Upatanisho aliyoanza kufanya Kristo mwaka 1844 katika chumba cha pili cha Hekalu la mbinguni kinachoitwa Patakatifu pa Patakatifu (Ebr. 9:23-26; Ufu. 11:19). Akimaliza atatamka maneno ya kutisha sana yatakayoamua umilele wa kila mmoja wetu, ama kwa uzima wa milele, ama kwa mauti ya milele, hapa ndipo uamuzi wako leo utakuamulia upande ambao utakuwa. (Ufu.22:11,12). Ndipo atakuja kuwachukua watu wake na kuwaangamiza waovu. Waovu ni watu gani leo ,? kwa ufupi wote tumepungukiwa na utukufu wa. Mungu ndio maana tunarudi miguuni pake kwa kuangalia mapito aliyopita na kuenenda katika maagizo yake ,usikubali kuendeshwa na mwanadamu hasa kwa maisha ya kiroho mruhusu Mungu mwenyewe akuongoze kupitia neno lake.
Somo la Patakatifu litafuata baada ya kumaliza unabii huu wa Daniel hilo somo ni mhimu sana linaonesha nini kinachoendelea kwa kila mwanadamu leo ambacho kikimalizika tayari nafasi tena ya Rehema haitakuwa na nafasi ,kumbuka Mpendwa hii nafasi ya kupata neno la Mungu itakuja kuwa na ukomo wake hivyo shika sana kila unachopata kwa unabii huu (Amos8:11-14) Bwana akubariki Karibu kwa sura inayofuata.
(SOMA DANIELI 8 YOTE)
Ninapenda kuwakaribisha katika muendelezo wakujifunza neno la Mungu hasa katika unabii wa Daniel, kwanza ninapenda kuweka wazi jambo hili ,hatufundishi kwa kushambulia dhehebu au dini bali tunasema yaliyo kweli hasa ,kwahiyo usidhani kuna mabishano ya hoja ,hapana tunasema na kweka huru ukweli ili mtu mwenyewe asome ,alinganishe na kufanya uamuzi yeye mwenyewe ,jambo jingine ni kwamba MUNGU huwa anawapa taarifa watu wake kabla ya maafa kuwapata ,kwahiyo haya ni maonyo kwa watu wake kuhusu yale ambayo yanaendelea iliyatakapo tokea asiwepo mtu atakayesema Mimi sikuyasikia ,wala sikuambiwa ili hukumu itakapokuja kila mtu aseme HAKIKA HUKUMU ZAKO NI ZA HAKI NAZA KWELI .
Kwahiyo hatutoi mafundisho kwa kujaribu tunatoa ukweli kama ulivyo ,ni kweli unapoguswa lazima utafute njia ya kujitetea lakini kumbuka wokovu ni maamuzi yako ,muda Utakuja ambapo neno la Mungu halitaonekana tena ,ninacho kushauri usichoke kujifunza neno la Mungu omba Mungu akufunulie zaidi ,utabarikiwa na uzima wa milele uaambatana nawe.
Kumbuka kama tulivyoona kuwa Pembe Ndogo ya Danieli 7 inawakilisha Ufalme wa Papa. Lakini Pembe Ndogo ya Danieli 8 inaziwakilisha falme mbili ----- Rumi ya Kipagani na Rumi ya Kipapa.
Ni sawa tu na lile Joka Kubwa Jekundu la Ufunuo 12 lenye vichwa saba na pembe kumi ambalo linaziwakilisha falme zizo hizo mbili. Utazitofautisha kwa vitendo vyake tu.
Mungu haoni tofauti yo yote kati ya Rumi ya Kipagani na Rumi ya Kipapa.
Yesu aliziita falme zote mbili "Chukizo la Uharibifu," yaani, Mamlaka Zinazowaangamiza watu wa Mungu (Mt. 24:15,22; Dan. 9:27). Danieli 8 na 9 ni kitu kimoja; Gabrieli alishindwa kuendelea kumweleza Danieli habari za Pembe hiyo Ndogo ambayo itawaua watakatifu kiasi cha kustaajabisha kwa vile alikuwa amezimia (Dan. 8:24,27).
Baada ya muda kupita Gabrieli alimjia tena Danieli akamwambia anataka kumpa ufahamu wa njozi ya Danieli 8 ambayo alikatisha kumweleza (Dan. 9:20-22). Lakini kwa urahisi wa kuelewa tutachukua kila sura peke yake. Katika sura ya 8 kuna maono ya aina mbili ----- Kondoo mume mwenye pembe mbili (Dan. 8:3,4) ambaye anawakilisha Ufalme wa Wamedi na Waajemi (Dan. 8:20); kisha akaona Beberu mwenye pembe mashuhuri kati ya macho yake (Dan. 8:5-8) ambaye anauwakilisha Ufalme wa Wayunani (Dan. 8:21). Ile pembe mashuhuri ni mtawala wa kwanza Iksanda Mkuu (Dan. 8:21). Zile pembe nne ni majemadari wake wanne waliotawala baada ya kufa kwake Iskanda Mkuu (Dan. 8:22). Cassander alitwaa Jimbo la Magharibi; Lysimachus Jimbo la Kaskazini; Seleucus Jimbo la Mashariki (Siria kwenda mashariki), Ptolemy Jimbo la Kusimi (Misri na visiwa).
Falme hizo za Kiyunani zilipigana zenyewe kwa zenyewe; hatimaye Seleucus akachukua eneo lote la mashariki, kaskazini, na magharibi baada ya kuwashinda wenzake.
Ni katika pembe (ufalme) ya Seleucus ilimotokea Pembe ile Ndogo ambayo inaiwakilisha Rumi ya Kipagani, na hatimaye Rumi ya Kipapa (Dan. 8:9). Kwa maneno mengine Ufalme wa Warumi ulitokea katika eneo la Seleucus alilotawala.
Hiyo ni kweli kijiografia na kihistoria. Sasa tutaangalia mambo machache tu juu ya kazi iliyofanywa na Pembe hiyo Ndogo ya Danieli 8. Mungu kwa mkono wa Musa alikuwa amewaonya Waisraeli kuwa atawaletea taifa ambalo lugha yake hawaijui, litawazingira, watakula watoto wao; hayo yalitokea mwaka wa 70 B.K.
majeshi ya Warumi yalipouzingira Yerusalemu na kuuharibu kabisa pamoja na hekalu lake (Kum. 28:49-57; Dan. 9:26,27; Mt. 24:15-20; Luka 21:20-24). Ukatili wa falme hizo zinazowakilishwa na "mfalme mwenye uso mkali", yaani, katili, umedokezwa (Dan. 8:23,24). Wayahudi walijua Kiyunani lakini sio Kilatini. Agano jipya liliandikwa kwa Kiyunani, lugha ya Dola ya Wayunani.
Falme zote mbili, Rumi ya Kipagani na Rumi ya Kipapa zilitumia hila katika kutawala kwao (Dan. 8:25). Soma Historia ya Kale. Mpaka hapo ni mambo ya jumla. Sasa na tuangalie vitendo vya falme hizo kwa uchache tu:
RUMI YA KIPAGANI:
Pembe Ndogo ilikua sana kuelekea nchi ya uzuri, yaani, Palestina (Dan. 8:9). Palestina ilichukuliwa na kuwa sehemu ya Rumi ya Kipagani mwaka 63 K.K. "Jeshi la mbinguni" ni watu wa Mungu, "nyota" ni viongozi wa dini (Dan. 8:10: Ufu. 1:20). "Kuangusha chini na kukanyaga" ni kuangamiza au kuua. Ufalme huu ulitimiza hayo mwaka 70 B.K. ulipouangamiza Mji wa Yerusalemu, kisha katika karne ya pili uliua wakristo wengi chini ya Kaisari Diocletian wa Rumi.
Hata kabla yake wakati wa Nero mauaji ya Wakristo yalifanyika. Historia inaweka idadi ya waliouawa na Rumi ya Kipagani takriban milioni 3. "Patakatifu pakaangushwa chini" ni kuliharibu hekalu mwaka 70 B.K. (Dan. 8:11). "Mkuu wa Jeshi" au "Mkuu wa wakuu" ni Kristo mwenyewe (Dan. 12:1. Ufu. 12:7,8; Yoshua 5:13-15; Ufu. 1:5). Neno "malaika" maana yake "mjumbe". Linaweza kutumika kwa Kristo na kwa viumbe wale wa mbinguni tunaowaita malaika (Ebr. 1:14), au kwa "wachungaji" (Ufu. 2:1,8,12,18; 3:1,7). "Mikaeli" ni jina la Yesu anapokuwa Mkuu wa Majeshi ya Malaika (Amiri Jeshi wa Jeshi la Bwana).
Sauti yake ndiyo itakayowafufua wafu (Yoh. 5:25,28,29; 1 The. 4:16), anaitwa Malaika Mkuu. Huyo Pilato, Gavana wa Rumi ya Kipagani, alikabiliana naye ana kwa ana kama ilivyotabiriwa katika Dan. 8:11,25 (Yoh. 18:33-37; 19:1-3,10,11,23,19-22). Alisulibiwa juu ya msalaba wa Kirumi; alipigwa kwa mijeledi ya Kirumi, na kupigiliwa kwa misumari ya Kirumi, na kaburi lake likalindwa na askari wa Kirumi. Unabii huo ulitimia mia kwa mia.
RUMI YA KIPAPA:
Tutaangalia mambo kadhaa tu, sio yote. Rumi ya Kipapa ili"iangusha kweli hata chini" (Dan. 8:12). Kweli ni nini? Kweli ni Neno la Mungu, kweli ni Sheria ya Mungu (Amri Kumi). Soma Yoh. 17:17; Zab. 119:142. Upapa umeikanyaga chini ya miguu yake Sheria ya Amri Kumi kwa kufuta Amri ya pili inayokataza ibada ya sanamu, na kuweka Jumapili badala ya Sabato (Jumamosi) kama siku ya ibada (Dan. 7:25; Ufu. 13:16,17). Jumapili katika unabii inaitwa "Chapa au Alama ya Mnyama", yaani, Alama ya Uwezo wa Mamlaka ya Papa.
Sabato inaitwa Muhuri wa Mungu (Ufu. 7:1-4) au "Alama ya Mungu" (Eze. 9:4-11).
Martin Luther aligundua makosa (mafundisho potofu) 95. Sasa ni zaidi kuliko hayo. "Kukanyagisha patakatifu na jeshi"; yeye hajaliangusha jengo la hekalu, ila amegeuza mawazo ya waumini kumwelekea yeye badala ya Kuhani Mkuu, Yesu Kristo, katika Hekalu la Mbinguni kwa kuanzisha ukuhani na misa (Ebr. 4:14-16; 3:1). Kosa lingine ni lile la kutumia cheo cha Mungu cha "Baba Mtakatifu" (Yoh. 17:11). Muda hautoshi kuorodhesha mafundisho potofu yanayoitwa "mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake" (Ufu. 14:8; 17:2). Unafundisha Mapokeo badala ya Biblia (Mt. 15:3-9; Marko 7:5-13). Uliua watakatifu zaidi ya milioni 50 katika kipindi chake cha utawala wa miaka 1260 (538-1798), kiitwacho Zama za Giza (Dan. 8:24,25; Mt. 24:21,22). Waliomo katika mfumo huo wa utawala wanaambiwa watoke (Ufu. 18:4,5). Maana yake watoke katika kuabudu bila kufuata maagizo ya Mungu namna ambayo wanasema kuabudu ,hapa watu wote kuanzia anayekalia kiti cha papa hadi mlei wanatakiwa watoke katika huo mfumo maana mungu mwenyewe wanasema watoke .Na mamilioni watatoka kwa dhiki kubwa pamoja na kuuawa na wale watakaobaki katika mfumo huo (Ufu. 15:2; 20:4). Katika Danieli 7:9,10 hukumu ilifuatia baada ya upapa kufanya kazi yake kwa miaka 1260. Hapa pia tunaona hukumu ile ile ikirudiwa kwa maneno haya: "Hata nyakati za jioni na asubuhi elfu mbili na mia tatu; ndipo patakatifu patakapotakaswa" (Dan. 8:14). hili somo nitalitolea Maelezo baada ya hili kuisha ,na somo la patakatifu litafuaata. Mpango wote wa wokovu umedhihirishwa katika Hekalu la duniani na lile la Mbinguni (Ebr. 8:1,2; 9:6,7; Law. 16 yote; Law. 23:27-32). Tangu Sinai hadi Yesu alipokata roho msalabani huduma hiyo iliendeshwa na makuhani pamoja na kuhani mkuu na kufikia mwisho wake (Kut. 25:8; Mt. 27:50,51).
Yesu alipopaa mwaka 31 B.K. alikwenda moja kwa moja katika huduma ya chumba cha kwanza cha Hekalu la mbinguni (Ebr. 9:11,12) kama Kuhani Mkuu.
Siku 2300 za Dan. 8:14 ni siku za unabii, ni sawa na miaka 2300 (Eze. 4:6). Zilianza kuhesabiwa wakati ule amri ya kuujenga upya Yerusalemu ilipotolewa mwaka 457 K.K. na kukoma 1844 B.K. Kutakaswa kwa Patakatifu ni kazi ya Hukumu au Utakaso au Upatanisho aliyoanza kufanya Kristo mwaka 1844 katika chumba cha pili cha Hekalu la mbinguni kinachoitwa Patakatifu pa Patakatifu (Ebr. 9:23-26; Ufu. 11:19). Akimaliza atatamka maneno ya kutisha sana yatakayoamua umilele wa kila mmoja wetu, ama kwa uzima wa milele, ama kwa mauti ya milele, hapa ndipo uamuzi wako leo utakuamulia upande ambao utakuwa. (Ufu.22:11,12). Ndipo atakuja kuwachukua watu wake na kuwaangamiza waovu. Waovu ni watu gani leo ,? kwa ufupi wote tumepungukiwa na utukufu wa. Mungu ndio maana tunarudi miguuni pake kwa kuangalia mapito aliyopita na kuenenda katika maagizo yake ,usikubali kuendeshwa na mwanadamu hasa kwa maisha ya kiroho mruhusu Mungu mwenyewe akuongoze kupitia neno lake.
Somo la Patakatifu litafuata baada ya kumaliza unabii huu wa Daniel hilo somo ni mhimu sana linaonesha nini kinachoendelea kwa kila mwanadamu leo ambacho kikimalizika tayari nafasi tena ya Rehema haitakuwa na nafasi ,kumbuka Mpendwa hii nafasi ya kupata neno la Mungu itakuja kuwa na ukomo wake hivyo shika sana kila unachopata kwa unabii huu (Amos8:11-14) Bwana akubariki Karibu kwa sura inayofuata.
1 comments:
Click here for commentsBwana Yesu asifiwe!
nimejaribu kupitia masomo uliyoyaweka kwenye blog yako
Mungu akubariki maradufu
naweza pata no yako?
ConversionConversion EmoticonEmoticon