Ninachukua hii nafasi kukuarika tena mpendwa na rafiki katika kujifunza neno la Mungu ,ukiangalia kwa umakini hata sasa kuna mambo mengi yanayoendelea hapa duniani ,ukiangalia kila kukicha mambo mapya mengi yanaibuka rafiki usishangae hata tukio la hivi karibuni juu ya raisi wa marekani kuutambua yerusalemu kama mji mkuu ya israeli haya yote hayatokei bila kuwa katika mpango au kujurikana hapo awali ,mambo yote yanayofanyika hayafanyiki kwa bahati mbaya bali yako katika mpangilio ,ueipate shaka nitakuletea matukio ya siku hizi kwa uwazi kabisa ,karibu kwa masomo haya ,
Mgunduzi wa Mafundisho ya Uongo ni shetani ,hapo awali Shetani alijua fika ya kwamba Maandiko yale Matakatifu yangewawezesha wanadamu kuyang’amua madanganyo yake na kuupinga uwezo wake.
Ilikuwa ni kwa njia ya Neno hilo hata yule Mwokozi wa ulimwengu aliweza kuyapinga mashambulio yake. Kwa kila shambulio lake [Shetani], Kristo alionyesha ngao ya ile kweli ya milele, akisema, “Imeandikwa.” Kwa kila shauri alilotoa yule adui, alikataa kwa kutegemea hekima na uwezo wa lile neno. Ili huyo Shetani apate kudumisha utawala wake juu ya wanadamu, na kuimarisha mamlaka ya tapeli yule wa kipapa, ilikuwa ni lazima kwake kuwaweka watu katika hali ya ujinga wa kutoyajua Maandiko. Biblia ingemtukuza Mungu na kuwaweka wanadamu mahali pao panapowastahili hasa; kwa hiyo ilikuwa ni lazima kwamba zile kweli zake takatifu zifichwe kwa watu na kupigwa marufuku. Mantiki hiyo ikatumiwa na Kanisa la Roma.
Kwa mamia ya miaka uenezaji wa Biblia ulipigwa marufuku. Watu walikatazwa kuisoma au kuwa nayo katika nyumba zao, na makasisi (mapadre) pamoja na maaskofu wapotovu wakayafafanua mafundisho yake ili yapate kuunga mkono unafiki wao. Hivyo ndivyo papa alivyokuja kutambulikana karibu ulimwenguni kote kama Kaimu wa [Aliye Badala ya] Mungu hapa duniani, ambaye alipewa mamlaka juu ya kanisa na serikali.Kuupigia Magoti Upagani Baada ya kuondolewa yule anayegundua mafundisho potofu [yaani, Biblia], Shetani akafanya kama apendavyo. Unabii ulikuwa umetangaza kwamba upapa unge“azimu kubadili majira na Sheria [Amri Kumi].” Danieli 7:25. Kazi hiyo [upapa] haukuchelewa kuanza kuifanya. Ili kuwapa waongofu waliotoka kwenye upagani kitu fulani badala ya ibada yao ya sanamu, na kukuzia upokeaji wao wa Ukristo kwa jina tu, kuabudu sanamu na mabaki ya mifupa ya watakatifu waliokufa zamani vikaingizwa taratibu katika ibada ya Kikristo. Amri iliyotolewa na baraza kuu hatimaye ikauimarisha mfumo huo wa ibada ya sanamu. Kuikamilisha kazi hiyo ya kukufuru, Roma ikadhamiria kuifutilia mbali kutoka katika Sheria ya Mungu [Amri Kumi] amri ile ya pili inayokataza ibada ya sanamu, na kuigawa amri ile ya kumi ili kuhifadhi idadi ile ile [ya Amri Kumi]
SHERIA YA MUNGU
I -Usiwe na miungu mingine ila mimi.
II -Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu Mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia. Usivisujudu wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, BWANA, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, nami nawarehemu maelfu elfu Wanipendao, na kuzishika amri zangu.
III -Usilitaje bure jina la BWANA, Mungu wako, maana BWANA hatamhesabia kuwa hana hatia mtu alitajaye jina lake bure.
IV -Ikumbuke siku ya Sabato uitakase. Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote; Lakini siku ya saba ni Sabato ya BWANA, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako. Maana, kwa siku sita BWANA alifanya Mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; Kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa.
V -Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na BWANA, Mungu wako.
VI- Usiue.
VII- Usizini.
VIII -Usiibe.
IX -Usimshuhudie jirani yako uongo.
X- Usiitamani nyumba ya jirani yako, usimtamani mke wa jirani yako, mtumwa wake, wala mjakazi , wala ng’ombe wake, wala punda wake, wala cho chote alicho nacho jirani yako. Kutoka 20:3-17
SHERIA YA MUNGU KAMA ILIVYOBADILISHWA NA MWANADAMU
I - Mimi ni Bwana Mungu wako, Usiwe na miungu migeni ila mimi. (Amri ya Pili Imeachwa.)
II- (Hii hasa ni ya III) Usilitaje bure jina la Bwana, Mungu wako.
III- (Hii hasa ni ya IV) Kumbuka kwamba unaitakasa siku ya Sabato. (Amri ya Sabato imebadilishwa vibaya sana!)
IV- (Hii hasa ni ya V) Waheshimu baba na mama yako.
V- (Hii hasa ni ya VI) Usiue.
VI- (Hii hasa ni ya VII)Usizini
VII- (Hii hasa ni ya VIII) Usiibe.
VIII- (Hii hasa ni ya IX) Usimshuhudie jirani yako uongo.
IX- (Hii hasa ni ya X, Sehemu ya Kwanza) Usimtamani mke wa jirani yako.
X- (Hii hasa ni ya X, Sehemu ya Pili) Usitamani mali ya jirani yako.
Katekisimu ya Wote ya Kikatoliki
Maridhiano Yaendelea
Roho ile ya maridhiano na upagani ikafungua njia ya kutoijali sana Mamlaka ile ya Mbinguni.
Shetani, akifanya kazi yake kwa kuwatumia viongozi wa kanisa wasiojitoa wakf kwa Mungu, akaigeuza amri ile ya nne pia, na kujaribu kuiweka kando Sabato ile ya kale [Jumamosi], siku ambayo Mungu alikuwa ameibarikia na kuitakasa, na mahali pake kuitukuza sikukuu iliyoadhimishwa na makafiri kama “siku tukufu ya jua” [Jumapili].
Badiliko hilo mwanzoni halikufanywa waziwazi.
Katika karne zile za mwanzo Sabato ya kweli [Jumamosi] ilikuwa imetunzwa na Wakristo wote. Walikuwa na wivu kwa ajili ya heshima ya Mungu, na, wao wakiwa wanaamini kwamba Sheria ya Mungu [Amri Kumi] haibadiliki kamwe, basi, kwa bidii nyingi walitunza utakatifu wa amri zake [kumi].
Lakini kwa usiri mkubwa Shetani alifanya kazi yake kupitia kwa vibaraka wake ili kutekeleza lengo lake. Ili mawazo ya watu yapate kugeuzwa kuelekea kwenye ile Jumapili, ikafanywa kuwa sikukuu ya kuheshimu ufufuo wa Kristo.
Ibada za dini zikaendeshwa kataika siku hiyo; lakini bado ilifikiriwa kama siku ya mapumziko tu, Sabato [Jumamosi] ikiwa inaendelea kutakaswa.
Kutayarisha njia kwa ajili ya kazi ile aliyokusudia kuifanya,
Shetani akawaongoza Wayahudi, kabla ya kuja kwa Kristo, kuiwekea Sabato mizigo mizito na masharti makali, wakifanya utunzaji wake kuwa mzigo mzito ulemeao.
Basi, [Shetani] akiitumia nafasi hiyo ya kuwapo kwa nuru ile ya uongo ambayo kwayo aliifanya [Sabato] ifikiriwe vibaya, akaifanya ipate kudharauliwa na watu kama siku ya Wayahudi, Wakati Wakristo wakiendelea kwa kawaida kuiadhimisha Jumapili kama sikukuu ya furaha, akawaongoza kuifanya siku ya Sabato [Jumamosi] kuwa siku ya kufunga [saumu], yaani, siku ya huzuni na majonzi, ili kuonyesha chuki yao dhidi ya dini ile ya Kiyahudi
Badiliko la Kijasiri
Katika sehemu ile ya kwanza ya karne ya nne mfalme Konstantino alitoa amri na kuifanya Jumapili kuwa sikukuu ya serikali katika dola yote ya Waroma. Siku hiyo ya jua [Jumapili] iliheshimiwa na raia zake wapagani, tena iliheshimiwa na Wakristo; ilikuwa ni sera ya mfalme yule kuunganisha mambo yale waliyoyapenda makafiri na Wakristo ambayo yalikuwa yanaleta mgongano. Alishurutishwa kufanya hivyo na maaskofu wa kanisa, wakiwa wamechochewa na tamaa ya ukuu na kiu ya mamlaka walitambua kwamba kama siku ile ile moja ingeadhimishwa na Wakristo na makafiri, basi, ingeweza kusaidia kupokelewa kwa Ukristo na wapagani wale na kwa njia hiyo kuendeleza mbele mamlaka na utukufu wa kanisa.
Lakini Wakristo wengi wacha Mungu waliposhawishiwa polepole kuifikiria Jumapili kama ina kiwango fulani cha utakatifu, bado waliendelea kuitunza Sabato ya kweli [Jumamosi] kama takatifu kwa Bwana, tena waliitunza kwa kutii amri ile ya nne [Kut. 20:8-11].
Laghai yule mkuu [Shetani] alikuwa bado hajaikamilisha kazi yake. Akaazimu kuukusanya pamoja Ulimwengu wote wa Kikristo chini ya bendera yake na kutumia uwezo wake kupitia kwa kaimu wake, yaani, yule papa, mwenye majivuno mengi, aliyejidai kwamba alikuwa ndiye mwakilishi wake Kristo.
Kupitia kwa wapagani wale walioongoka nusu-nusu, na kwa maaskofu wale wenye kutaka makuu, na kwa watu wa kanisa walioipenda dunia akalitimiza kusudi lake.
Mabaraza makubwa sana yakafanywa toka wakati hata wakati, na katika hayo viongozi wakuu wa kanisa walikutana kutoka pande zote za ulimwengu. Karibu katika kila baraza lililokaa, Sabato [Jumamosi] ambayo Mungu alikuwa ameianzisha ikasukumiwa chini kidogo zaidi, wakati ule ule Jumapili ikawa inainuliwa juu.
Hivyo ndivyo sikukuu ile ya kipagani [Jumapili] ilivyokuja kuheshimiwa hatimaye kama siku iliyowekwa na Mungu, na wakati ule ule Sabato ile ya Biblia [Jumamosi] ikatangazwa kuwa ilikuwa ni mabaki ya dini ile ya Kiyahudi, na watunzaji wake wakatangazwa kuwa wamelaaniwa.
Soma hii rejea
"Jumapili imewekwa na Wakatoliki, na madai ya kutaka itunzwe yanaweza tu kutetewa kwa kufuata kanuni za Kikatoliki….Toka mwanzo hadi mwisho wa Maandiko Matakatifu hakuna kifungu hata kimoja kinachotoa kibali cha kuhamisha ibada ya kila juma kutoka katika siku ile ya mwisho wa juma kwenda ile ya kwanza." Catholic Press, Sydney, Australia, Agosti, 1900.
Muhuri wa Muumbaji Waondolewa
Mwasi huyo mkuu alikuwa amefanikiwa kujiinua mwenyewe “juu ya kila kiitwacho Mungu ama kuabudiwa.” 2 Wathesalonike 2:4. Akadiriki kuibadili amri ile ya pekee katika Sheria ya Mungu [Amri Kumi] ambayo bila kukosea hata kidogo inawaelekeza wanadamu wote kwa Mungu wa kweli, aliye hai. Katika amri ile ya nne [Kut. 20:8-11]
Mungu anadhihirishwa kama ndiye Muumbaji wa mbingu na nchi, na kwa sababu hiyo yeye anatofautishwa na miungu yote ya uongo.
Ilikuwa ni kwa ajili ya kumbukumbu ya kazi ile ya uumbaji, ndiyo maana siku ile ya saba [Jumamosi] ilitakaswa [ilitengwa kwa matumizi matakatifu] kama siku ya mapumziko kwa kila mwanadamu. Ilikusudiwa kumweka Mungu aliye hai daima kataika mawazo ya wanadamu kama chimbuko la uhai wao na lengo la kicho chao na ibada yao.
Shetani anajitahidi sana iuwageuza watu waache kumtii Mungu, na kuacha kutoa utii wao kwa Sheria yake [Amri Kumi]; kwa hiyo, juhudi zake anazielekeza hasa dhidi ya amri ile [ya Sabato] inayomwonyesha Mungu kuwa ni Muumbaji. Waprotestanti siku hizi wanasisitiza kwamba ufufuo wake Kristo katika siku ile ya Jumapili ndio ulioifanya siku hiyo kuwa Sabato ya Kikristo. Lakini ushahidi wa Maandiko unakosekana. Hakuna heshima kama hiyo iliyotolewa kwa siku hiyo [ya Jumapili] na Kristo au na Mitume wake.kiukweli Hakuna hiyo rejea kimaandiko bali hutumia kigezo cha kufufuka kwa Kristo ,ndugu rafiki ukweli huweka huru ,yohana 17:17 hufungua kutoka madhakani ,ninakuarika uendelee kufuatilia haya masomo na mengine yapo tayari katika hii blogspot waweza kujifunza zaidi, lakini ninakuomba usichoke kujifunza neno la Mungu yeye atakuongoza katika hii kweli ,daima omba zaidi ,soma neno kisha jitoe kumfuata hautapungukiwa hata kuurithi uzima wa milele ,Mungu akubariki Karibu kwa somo linalofuata .
Mgunduzi wa Mafundisho ya Uongo ni shetani ,hapo awali Shetani alijua fika ya kwamba Maandiko yale Matakatifu yangewawezesha wanadamu kuyang’amua madanganyo yake na kuupinga uwezo wake.
Ilikuwa ni kwa njia ya Neno hilo hata yule Mwokozi wa ulimwengu aliweza kuyapinga mashambulio yake. Kwa kila shambulio lake [Shetani], Kristo alionyesha ngao ya ile kweli ya milele, akisema, “Imeandikwa.” Kwa kila shauri alilotoa yule adui, alikataa kwa kutegemea hekima na uwezo wa lile neno. Ili huyo Shetani apate kudumisha utawala wake juu ya wanadamu, na kuimarisha mamlaka ya tapeli yule wa kipapa, ilikuwa ni lazima kwake kuwaweka watu katika hali ya ujinga wa kutoyajua Maandiko. Biblia ingemtukuza Mungu na kuwaweka wanadamu mahali pao panapowastahili hasa; kwa hiyo ilikuwa ni lazima kwamba zile kweli zake takatifu zifichwe kwa watu na kupigwa marufuku. Mantiki hiyo ikatumiwa na Kanisa la Roma.
Kwa mamia ya miaka uenezaji wa Biblia ulipigwa marufuku. Watu walikatazwa kuisoma au kuwa nayo katika nyumba zao, na makasisi (mapadre) pamoja na maaskofu wapotovu wakayafafanua mafundisho yake ili yapate kuunga mkono unafiki wao. Hivyo ndivyo papa alivyokuja kutambulikana karibu ulimwenguni kote kama Kaimu wa [Aliye Badala ya] Mungu hapa duniani, ambaye alipewa mamlaka juu ya kanisa na serikali.Kuupigia Magoti Upagani Baada ya kuondolewa yule anayegundua mafundisho potofu [yaani, Biblia], Shetani akafanya kama apendavyo. Unabii ulikuwa umetangaza kwamba upapa unge“azimu kubadili majira na Sheria [Amri Kumi].” Danieli 7:25. Kazi hiyo [upapa] haukuchelewa kuanza kuifanya. Ili kuwapa waongofu waliotoka kwenye upagani kitu fulani badala ya ibada yao ya sanamu, na kukuzia upokeaji wao wa Ukristo kwa jina tu, kuabudu sanamu na mabaki ya mifupa ya watakatifu waliokufa zamani vikaingizwa taratibu katika ibada ya Kikristo. Amri iliyotolewa na baraza kuu hatimaye ikauimarisha mfumo huo wa ibada ya sanamu. Kuikamilisha kazi hiyo ya kukufuru, Roma ikadhamiria kuifutilia mbali kutoka katika Sheria ya Mungu [Amri Kumi] amri ile ya pili inayokataza ibada ya sanamu, na kuigawa amri ile ya kumi ili kuhifadhi idadi ile ile [ya Amri Kumi]
SHERIA YA MUNGU
I -Usiwe na miungu mingine ila mimi.
II -Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu Mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia. Usivisujudu wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, BWANA, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, nami nawarehemu maelfu elfu Wanipendao, na kuzishika amri zangu.
III -Usilitaje bure jina la BWANA, Mungu wako, maana BWANA hatamhesabia kuwa hana hatia mtu alitajaye jina lake bure.
IV -Ikumbuke siku ya Sabato uitakase. Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote; Lakini siku ya saba ni Sabato ya BWANA, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako. Maana, kwa siku sita BWANA alifanya Mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; Kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa.
V -Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na BWANA, Mungu wako.
VI- Usiue.
VII- Usizini.
VIII -Usiibe.
IX -Usimshuhudie jirani yako uongo.
X- Usiitamani nyumba ya jirani yako, usimtamani mke wa jirani yako, mtumwa wake, wala mjakazi , wala ng’ombe wake, wala punda wake, wala cho chote alicho nacho jirani yako. Kutoka 20:3-17
SHERIA YA MUNGU KAMA ILIVYOBADILISHWA NA MWANADAMU
I - Mimi ni Bwana Mungu wako, Usiwe na miungu migeni ila mimi. (Amri ya Pili Imeachwa.)
II- (Hii hasa ni ya III) Usilitaje bure jina la Bwana, Mungu wako.
III- (Hii hasa ni ya IV) Kumbuka kwamba unaitakasa siku ya Sabato. (Amri ya Sabato imebadilishwa vibaya sana!)
IV- (Hii hasa ni ya V) Waheshimu baba na mama yako.
V- (Hii hasa ni ya VI) Usiue.
VI- (Hii hasa ni ya VII)Usizini
VII- (Hii hasa ni ya VIII) Usiibe.
VIII- (Hii hasa ni ya IX) Usimshuhudie jirani yako uongo.
IX- (Hii hasa ni ya X, Sehemu ya Kwanza) Usimtamani mke wa jirani yako.
X- (Hii hasa ni ya X, Sehemu ya Pili) Usitamani mali ya jirani yako.
Katekisimu ya Wote ya Kikatoliki
Maridhiano Yaendelea
Roho ile ya maridhiano na upagani ikafungua njia ya kutoijali sana Mamlaka ile ya Mbinguni.
Shetani, akifanya kazi yake kwa kuwatumia viongozi wa kanisa wasiojitoa wakf kwa Mungu, akaigeuza amri ile ya nne pia, na kujaribu kuiweka kando Sabato ile ya kale [Jumamosi], siku ambayo Mungu alikuwa ameibarikia na kuitakasa, na mahali pake kuitukuza sikukuu iliyoadhimishwa na makafiri kama “siku tukufu ya jua” [Jumapili].
Badiliko hilo mwanzoni halikufanywa waziwazi.
Katika karne zile za mwanzo Sabato ya kweli [Jumamosi] ilikuwa imetunzwa na Wakristo wote. Walikuwa na wivu kwa ajili ya heshima ya Mungu, na, wao wakiwa wanaamini kwamba Sheria ya Mungu [Amri Kumi] haibadiliki kamwe, basi, kwa bidii nyingi walitunza utakatifu wa amri zake [kumi].
Lakini kwa usiri mkubwa Shetani alifanya kazi yake kupitia kwa vibaraka wake ili kutekeleza lengo lake. Ili mawazo ya watu yapate kugeuzwa kuelekea kwenye ile Jumapili, ikafanywa kuwa sikukuu ya kuheshimu ufufuo wa Kristo.
Ibada za dini zikaendeshwa kataika siku hiyo; lakini bado ilifikiriwa kama siku ya mapumziko tu, Sabato [Jumamosi] ikiwa inaendelea kutakaswa.
Kutayarisha njia kwa ajili ya kazi ile aliyokusudia kuifanya,
Shetani akawaongoza Wayahudi, kabla ya kuja kwa Kristo, kuiwekea Sabato mizigo mizito na masharti makali, wakifanya utunzaji wake kuwa mzigo mzito ulemeao.
Basi, [Shetani] akiitumia nafasi hiyo ya kuwapo kwa nuru ile ya uongo ambayo kwayo aliifanya [Sabato] ifikiriwe vibaya, akaifanya ipate kudharauliwa na watu kama siku ya Wayahudi, Wakati Wakristo wakiendelea kwa kawaida kuiadhimisha Jumapili kama sikukuu ya furaha, akawaongoza kuifanya siku ya Sabato [Jumamosi] kuwa siku ya kufunga [saumu], yaani, siku ya huzuni na majonzi, ili kuonyesha chuki yao dhidi ya dini ile ya Kiyahudi
Badiliko la Kijasiri
Katika sehemu ile ya kwanza ya karne ya nne mfalme Konstantino alitoa amri na kuifanya Jumapili kuwa sikukuu ya serikali katika dola yote ya Waroma. Siku hiyo ya jua [Jumapili] iliheshimiwa na raia zake wapagani, tena iliheshimiwa na Wakristo; ilikuwa ni sera ya mfalme yule kuunganisha mambo yale waliyoyapenda makafiri na Wakristo ambayo yalikuwa yanaleta mgongano. Alishurutishwa kufanya hivyo na maaskofu wa kanisa, wakiwa wamechochewa na tamaa ya ukuu na kiu ya mamlaka walitambua kwamba kama siku ile ile moja ingeadhimishwa na Wakristo na makafiri, basi, ingeweza kusaidia kupokelewa kwa Ukristo na wapagani wale na kwa njia hiyo kuendeleza mbele mamlaka na utukufu wa kanisa.
Lakini Wakristo wengi wacha Mungu waliposhawishiwa polepole kuifikiria Jumapili kama ina kiwango fulani cha utakatifu, bado waliendelea kuitunza Sabato ya kweli [Jumamosi] kama takatifu kwa Bwana, tena waliitunza kwa kutii amri ile ya nne [Kut. 20:8-11].
Laghai yule mkuu [Shetani] alikuwa bado hajaikamilisha kazi yake. Akaazimu kuukusanya pamoja Ulimwengu wote wa Kikristo chini ya bendera yake na kutumia uwezo wake kupitia kwa kaimu wake, yaani, yule papa, mwenye majivuno mengi, aliyejidai kwamba alikuwa ndiye mwakilishi wake Kristo.
Kupitia kwa wapagani wale walioongoka nusu-nusu, na kwa maaskofu wale wenye kutaka makuu, na kwa watu wa kanisa walioipenda dunia akalitimiza kusudi lake.
Mabaraza makubwa sana yakafanywa toka wakati hata wakati, na katika hayo viongozi wakuu wa kanisa walikutana kutoka pande zote za ulimwengu. Karibu katika kila baraza lililokaa, Sabato [Jumamosi] ambayo Mungu alikuwa ameianzisha ikasukumiwa chini kidogo zaidi, wakati ule ule Jumapili ikawa inainuliwa juu.
Hivyo ndivyo sikukuu ile ya kipagani [Jumapili] ilivyokuja kuheshimiwa hatimaye kama siku iliyowekwa na Mungu, na wakati ule ule Sabato ile ya Biblia [Jumamosi] ikatangazwa kuwa ilikuwa ni mabaki ya dini ile ya Kiyahudi, na watunzaji wake wakatangazwa kuwa wamelaaniwa.
Soma hii rejea
"Jumapili imewekwa na Wakatoliki, na madai ya kutaka itunzwe yanaweza tu kutetewa kwa kufuata kanuni za Kikatoliki….Toka mwanzo hadi mwisho wa Maandiko Matakatifu hakuna kifungu hata kimoja kinachotoa kibali cha kuhamisha ibada ya kila juma kutoka katika siku ile ya mwisho wa juma kwenda ile ya kwanza." Catholic Press, Sydney, Australia, Agosti, 1900.
Muhuri wa Muumbaji Waondolewa
Mwasi huyo mkuu alikuwa amefanikiwa kujiinua mwenyewe “juu ya kila kiitwacho Mungu ama kuabudiwa.” 2 Wathesalonike 2:4. Akadiriki kuibadili amri ile ya pekee katika Sheria ya Mungu [Amri Kumi] ambayo bila kukosea hata kidogo inawaelekeza wanadamu wote kwa Mungu wa kweli, aliye hai. Katika amri ile ya nne [Kut. 20:8-11]
Mungu anadhihirishwa kama ndiye Muumbaji wa mbingu na nchi, na kwa sababu hiyo yeye anatofautishwa na miungu yote ya uongo.
Ilikuwa ni kwa ajili ya kumbukumbu ya kazi ile ya uumbaji, ndiyo maana siku ile ya saba [Jumamosi] ilitakaswa [ilitengwa kwa matumizi matakatifu] kama siku ya mapumziko kwa kila mwanadamu. Ilikusudiwa kumweka Mungu aliye hai daima kataika mawazo ya wanadamu kama chimbuko la uhai wao na lengo la kicho chao na ibada yao.
Shetani anajitahidi sana iuwageuza watu waache kumtii Mungu, na kuacha kutoa utii wao kwa Sheria yake [Amri Kumi]; kwa hiyo, juhudi zake anazielekeza hasa dhidi ya amri ile [ya Sabato] inayomwonyesha Mungu kuwa ni Muumbaji. Waprotestanti siku hizi wanasisitiza kwamba ufufuo wake Kristo katika siku ile ya Jumapili ndio ulioifanya siku hiyo kuwa Sabato ya Kikristo. Lakini ushahidi wa Maandiko unakosekana. Hakuna heshima kama hiyo iliyotolewa kwa siku hiyo [ya Jumapili] na Kristo au na Mitume wake.kiukweli Hakuna hiyo rejea kimaandiko bali hutumia kigezo cha kufufuka kwa Kristo ,ndugu rafiki ukweli huweka huru ,yohana 17:17 hufungua kutoka madhakani ,ninakuarika uendelee kufuatilia haya masomo na mengine yapo tayari katika hii blogspot waweza kujifunza zaidi, lakini ninakuomba usichoke kujifunza neno la Mungu yeye atakuongoza katika hii kweli ,daima omba zaidi ,soma neno kisha jitoe kumfuata hautapungukiwa hata kuurithi uzima wa milele ,Mungu akubariki Karibu kwa somo linalofuata .
ConversionConversion EmoticonEmoticon