Ndugu mpendwa huu ni muendelezo wa somo la patakatifu waweza kusoma somo la nyuma kupitia hii blog shuka chini utaona sehemu ya preveous hapo utayakuta ya nyuma yote.karibu tunapoendelea
Siku Kuu ya Upatanisho Kuhani mkuu aliingia katika patakatifu mno mara moja kwa mwaka ili kutakasa patakatifu.
Je mambo yalikuwaje wakati ule
Mbuzi wawili waliletwa na kupigiwa kura.
Kura moja kwa Bwana na kura moja kwa Azazeli.
Mbuzi wa Bwana alichinjwa kama sadaka ya dhambi kwa ajili ya watu. Na kuhani alichukua damu akaingia patakatifu mno, akainyunyiza kwenye kiti cha rehema na juu ya madhabahu ya uvumba. “Na haruni ataweka mikono yake miwili juu ya kichwa cha yule mbuzi aliye hai, na kuungama juu yake uovu wote wa wana wa Israeli, na makosa yao, naam, dhambi zao zote; naye ataziweka juu ya kichwa chake yule mbuzi, kisha atampeleka aende jangwani kwa mkono wa mtu aliye tayari.
Na yule mbuzi atachukua juu yake uovu wao wote, mpaka nchi isiyo watu; naye atamwacha mbuzi jangwani.” Law. 16:21-22. Huduma hiyo ilikusudiwa kuwaonyesha Waisraeli utakatifu wa Mungu, na jinsi anavyoichukia dhambi.
Kila mtu alitakiwa kujitakasa kwa njia ya kujichunguza wakati huduma hii inapokuwa ikiendeshwa.
Kazi zote na shughuli ziliachwa kabisa, na Waisraeli walitumia siku hiyo katika ibada na maombi, haliwakifunga na kujipeleleza mioyo yao na kuungama. Damu ya kafara ilikubaliwa badala ya mwenye dhambi kufa, lakini hatia ya dhambi haikufutwa kwa njia ya damu ya mnyama, ila ilihamishwa mpaka katika patakatifu.
Kule kutoa damu mwenye dhambi alikiri madaraka ya sheria, akaungama kuwa amevunja sheria, na akaamini na kuonyesha imani juu ya mkombozi atakayekuja, ambaye anafananishwa kwa mfano wa huduma hiyo. Walakini alikuwa hajafunguliwa kabisa atokane na hukumu ya kuvunja sheria.
Siku ya upatanisho kuhani mkuu akiisha kupokea sadaka ya watu, aliingia patakatifu mno. Alinyunyiza damu ya sadaka hiyo juu ya kiti cha rehema moja kwa moja kwenye sheria, ili kuiridhisha kwa kule kuvunjwa kwake. Halafu kama mwombezi alizichukua dhambi zote juu yake kutoka patakatifu.
Wakati anapoweka mikono yake juu ya yule mbuzi wa Azazeli huzihamisha dhambi hizo na kuziweka juu ya mbuzi. Basi mbuzi huzichukua zote. Ndipo kuhesabiwa kana kwamba zimetoweka milele, kutoka kwa watu. Ukweli wa Mbinguni Yale yaliyofanyika katika huduma ya patakatifu pa duniani, ambapo palikuwa kivuli cha yale ya mbinguni, ndivyo yalifanyika mbinguni ambako ndiko jambo halisi, katika patakatifu pa huko. Mwokozi wetu baada ya kufufuka kwake na kupaa mbinguni na kuanza kazi yake kama kuhani Mkuu.
“Kwa sababu Kristo hakuingia katika patakatifu palipofanyika kwa mikono, ndio mfano wa patakatifu halisi; bali aliingia mbinguni hasa, aonekane sasa usoni pa Mungu kwa ajili yetu”. Ebr. 9:24.
Huduma ya kuhani iliyokuwa ikifanyika katika chumba cha kwanza cha patakatifu, ni mfano wa huduma ya Kristo iliyoanza mbinguni baada ya kupaa kwake. Kuhani katika huduma yake ya kila siku, alileta damu ya sadaka mbele za Mungu, ambayo ni sadaka ya dhambi, pamoja na uvumba uliopaa juu pamoja na sala za watakatifu (Waisraeli). Vivyo hivyo Kristo aliombea damu yake mbele za Baba, kwa ajili ya wenye dhambi, na kuweka harufu njema ya haki yake mwenyewe mbele za Baba, sala za wenye kutubu makosa yao. Hiyo ilikuwa huduma iliyokuwa ikifanyika katika patakatifu, katika mbingu.
Hapo imani ya wanafunzi ilimfuata alipopaa juu, hapo matumaini yao yaliimarika, “tumaini tulilo nalo kama nanga ya rohoni, ambalo ni la hakika lililo imara” yaingiayo hata mle mlimo ndani ya pazia, alimoingia Yesu kwa ajili yetu, mtangulizi wetu amekuwa Kuhani Mkuu hata milele.
“Wala si kwa damu ya mbuzi na ndama, bali kwa damu yake mwenyewe aliingia mara moja tu katika patakatifu, akiisha kupata ukombozi wa milele”. Ebr. 6:19-20; 9:12.
Kwa muda wa karne kumi na nane kazi hiyo imekuwa ikifanyika mbinguni katika chumba cha kwanza cha patakatifu. Damu ya Kristo imeleta msamaha wa dhambi na kibali cha Baba cha kuwakubali wenye kutubu. Walakini dhambi zao bado zingali katika vitabu. Kama katika mfano ulivyo, kuna siku ya upatanisho kwa mwaka, vivyo hivyo kazi ya Kristo kwa ajili ya wanadamu haikamiliki mpaka kazi ya kulipa, au kafara ya malipo ifanyike. Kazi hiyo ni ya kuziondoa dhambi katika patakatifu.
Hii ilianza wakati siku 2300 zilipomalizika. Wakati huo Kuhani wetu Mkuu aliingia katika patakatifu mno ili kutakasa patakatifu.
Kazi ya Hukumu Katika agano jipya dhambi za watu wenye kutubu huwekwa juu ya Kristo, na kuhamishiwa mpaka katika patakatifu pa mbinguni. Na jinsi ilivyokuwa katika patakatifu pa duniani, dhambi zilikuwa zikiihamishwa kutoka patakatifu ili kukamilisha kazi, hali kadhalika na kutakasa patakatifu pa mbinguni patakamilika kwa njia hiyo hiyo ya kuhamisha dhambi kutoka vitabuni.
Kazi hii itakuwa kuangalia vitabu na kupima kuona ni nani ametubu kikweli na kuwa na imani kwa Kristo, ili afaidike kulipiwa adhabu yake kwa dhabihu ya Kristo. Kutakaswa kwa patakatifu basi ni kazi ya uchaguzi, kazi ya hukumu, kuona kuwa ni nani anastahili kupata uzima, na ni nani hastahili.
Kazi hii itafanyika kabla ya kuja kwa Kristo. Maana ajapo atakuja na ujira wake kumlipa kila mtu kama kazi yake itakavyokuwa. Ufunuo 22:12.
Hivyo wale waliofuata unabii unavyoelekeza, waliona kuwa badala ya Kristo kuja dunia mwisho wa siku 2300, yaani mwaka 1844, aliingia katika patakatifu pa patakatifu mbinguni ili kumaliza kazi yake ya uombezi na malipo ya adhabu kwa ajili ya dhambi, kabla ya kuja kwake duniani.
Dhambi zime samehewa juu ya kondoo na kuwekwa juu yake na katika damu ambayo huhamishwa na kupelekwa hekaluni. Sasa Kristo huzipokea dhambi na kuzihamisha katika hekalu la mbinguni.
Kristo akimaliza kuondoa dhambi za watu wake kutoka patakatifu pa mbinguni mwishoni mwa kazi yake ataziweka zote juu ya Shetani, atakayepata adhabu ya mwisho. Mbuzi wa Azazeli alipelekwa porini na kuachwa huko.
Hali kadhalika Shetani naye atatengwa mbali na Mungu milele, wala asionekane tena, kwa watu wa Mungu. Naye ataangamizwa kabisa, wala hatasalia na aina yoyote ya kumbukumbu. Wakati huo dhambi pia na wenye dhambi pia wataangamizwa milele.ndugu Mpendwa na rafiki katika Kristo ninakukaribisha katika kujitoa tungali bado katika kipindi hiki ,kabla YESU hajarudi kwa Mara ya pili atukute tuko tayari tukimngoja kama Bwana na mkombozi wetu .
Karibu sana tunapoendelea na sehemu inayofuata hasa katika unabii wa kitabu cha ufunuo.
Mungu akubariki sana.
Siku Kuu ya Upatanisho Kuhani mkuu aliingia katika patakatifu mno mara moja kwa mwaka ili kutakasa patakatifu.
Je mambo yalikuwaje wakati ule
Mbuzi wawili waliletwa na kupigiwa kura.
Kura moja kwa Bwana na kura moja kwa Azazeli.
Mbuzi wa Bwana alichinjwa kama sadaka ya dhambi kwa ajili ya watu. Na kuhani alichukua damu akaingia patakatifu mno, akainyunyiza kwenye kiti cha rehema na juu ya madhabahu ya uvumba. “Na haruni ataweka mikono yake miwili juu ya kichwa cha yule mbuzi aliye hai, na kuungama juu yake uovu wote wa wana wa Israeli, na makosa yao, naam, dhambi zao zote; naye ataziweka juu ya kichwa chake yule mbuzi, kisha atampeleka aende jangwani kwa mkono wa mtu aliye tayari.
Na yule mbuzi atachukua juu yake uovu wao wote, mpaka nchi isiyo watu; naye atamwacha mbuzi jangwani.” Law. 16:21-22. Huduma hiyo ilikusudiwa kuwaonyesha Waisraeli utakatifu wa Mungu, na jinsi anavyoichukia dhambi.
Kila mtu alitakiwa kujitakasa kwa njia ya kujichunguza wakati huduma hii inapokuwa ikiendeshwa.
Kazi zote na shughuli ziliachwa kabisa, na Waisraeli walitumia siku hiyo katika ibada na maombi, haliwakifunga na kujipeleleza mioyo yao na kuungama. Damu ya kafara ilikubaliwa badala ya mwenye dhambi kufa, lakini hatia ya dhambi haikufutwa kwa njia ya damu ya mnyama, ila ilihamishwa mpaka katika patakatifu.
Kule kutoa damu mwenye dhambi alikiri madaraka ya sheria, akaungama kuwa amevunja sheria, na akaamini na kuonyesha imani juu ya mkombozi atakayekuja, ambaye anafananishwa kwa mfano wa huduma hiyo. Walakini alikuwa hajafunguliwa kabisa atokane na hukumu ya kuvunja sheria.
Siku ya upatanisho kuhani mkuu akiisha kupokea sadaka ya watu, aliingia patakatifu mno. Alinyunyiza damu ya sadaka hiyo juu ya kiti cha rehema moja kwa moja kwenye sheria, ili kuiridhisha kwa kule kuvunjwa kwake. Halafu kama mwombezi alizichukua dhambi zote juu yake kutoka patakatifu.
Wakati anapoweka mikono yake juu ya yule mbuzi wa Azazeli huzihamisha dhambi hizo na kuziweka juu ya mbuzi. Basi mbuzi huzichukua zote. Ndipo kuhesabiwa kana kwamba zimetoweka milele, kutoka kwa watu. Ukweli wa Mbinguni Yale yaliyofanyika katika huduma ya patakatifu pa duniani, ambapo palikuwa kivuli cha yale ya mbinguni, ndivyo yalifanyika mbinguni ambako ndiko jambo halisi, katika patakatifu pa huko. Mwokozi wetu baada ya kufufuka kwake na kupaa mbinguni na kuanza kazi yake kama kuhani Mkuu.
“Kwa sababu Kristo hakuingia katika patakatifu palipofanyika kwa mikono, ndio mfano wa patakatifu halisi; bali aliingia mbinguni hasa, aonekane sasa usoni pa Mungu kwa ajili yetu”. Ebr. 9:24.
Huduma ya kuhani iliyokuwa ikifanyika katika chumba cha kwanza cha patakatifu, ni mfano wa huduma ya Kristo iliyoanza mbinguni baada ya kupaa kwake. Kuhani katika huduma yake ya kila siku, alileta damu ya sadaka mbele za Mungu, ambayo ni sadaka ya dhambi, pamoja na uvumba uliopaa juu pamoja na sala za watakatifu (Waisraeli). Vivyo hivyo Kristo aliombea damu yake mbele za Baba, kwa ajili ya wenye dhambi, na kuweka harufu njema ya haki yake mwenyewe mbele za Baba, sala za wenye kutubu makosa yao. Hiyo ilikuwa huduma iliyokuwa ikifanyika katika patakatifu, katika mbingu.
Hapo imani ya wanafunzi ilimfuata alipopaa juu, hapo matumaini yao yaliimarika, “tumaini tulilo nalo kama nanga ya rohoni, ambalo ni la hakika lililo imara” yaingiayo hata mle mlimo ndani ya pazia, alimoingia Yesu kwa ajili yetu, mtangulizi wetu amekuwa Kuhani Mkuu hata milele.
“Wala si kwa damu ya mbuzi na ndama, bali kwa damu yake mwenyewe aliingia mara moja tu katika patakatifu, akiisha kupata ukombozi wa milele”. Ebr. 6:19-20; 9:12.
Kwa muda wa karne kumi na nane kazi hiyo imekuwa ikifanyika mbinguni katika chumba cha kwanza cha patakatifu. Damu ya Kristo imeleta msamaha wa dhambi na kibali cha Baba cha kuwakubali wenye kutubu. Walakini dhambi zao bado zingali katika vitabu. Kama katika mfano ulivyo, kuna siku ya upatanisho kwa mwaka, vivyo hivyo kazi ya Kristo kwa ajili ya wanadamu haikamiliki mpaka kazi ya kulipa, au kafara ya malipo ifanyike. Kazi hiyo ni ya kuziondoa dhambi katika patakatifu.
Hii ilianza wakati siku 2300 zilipomalizika. Wakati huo Kuhani wetu Mkuu aliingia katika patakatifu mno ili kutakasa patakatifu.
Kazi ya Hukumu Katika agano jipya dhambi za watu wenye kutubu huwekwa juu ya Kristo, na kuhamishiwa mpaka katika patakatifu pa mbinguni. Na jinsi ilivyokuwa katika patakatifu pa duniani, dhambi zilikuwa zikiihamishwa kutoka patakatifu ili kukamilisha kazi, hali kadhalika na kutakasa patakatifu pa mbinguni patakamilika kwa njia hiyo hiyo ya kuhamisha dhambi kutoka vitabuni.
Kazi hii itakuwa kuangalia vitabu na kupima kuona ni nani ametubu kikweli na kuwa na imani kwa Kristo, ili afaidike kulipiwa adhabu yake kwa dhabihu ya Kristo. Kutakaswa kwa patakatifu basi ni kazi ya uchaguzi, kazi ya hukumu, kuona kuwa ni nani anastahili kupata uzima, na ni nani hastahili.
Kazi hii itafanyika kabla ya kuja kwa Kristo. Maana ajapo atakuja na ujira wake kumlipa kila mtu kama kazi yake itakavyokuwa. Ufunuo 22:12.
Hivyo wale waliofuata unabii unavyoelekeza, waliona kuwa badala ya Kristo kuja dunia mwisho wa siku 2300, yaani mwaka 1844, aliingia katika patakatifu pa patakatifu mbinguni ili kumaliza kazi yake ya uombezi na malipo ya adhabu kwa ajili ya dhambi, kabla ya kuja kwake duniani.
Dhambi zime samehewa juu ya kondoo na kuwekwa juu yake na katika damu ambayo huhamishwa na kupelekwa hekaluni. Sasa Kristo huzipokea dhambi na kuzihamisha katika hekalu la mbinguni.
Kristo akimaliza kuondoa dhambi za watu wake kutoka patakatifu pa mbinguni mwishoni mwa kazi yake ataziweka zote juu ya Shetani, atakayepata adhabu ya mwisho. Mbuzi wa Azazeli alipelekwa porini na kuachwa huko.
Hali kadhalika Shetani naye atatengwa mbali na Mungu milele, wala asionekane tena, kwa watu wa Mungu. Naye ataangamizwa kabisa, wala hatasalia na aina yoyote ya kumbukumbu. Wakati huo dhambi pia na wenye dhambi pia wataangamizwa milele.ndugu Mpendwa na rafiki katika Kristo ninakukaribisha katika kujitoa tungali bado katika kipindi hiki ,kabla YESU hajarudi kwa Mara ya pili atukute tuko tayari tukimngoja kama Bwana na mkombozi wetu .
Karibu sana tunapoendelea na sehemu inayofuata hasa katika unabii wa kitabu cha ufunuo.
Mungu akubariki sana.
ConversionConversion EmoticonEmoticon