TOKA ROMA YA KIPAGANI HADI YA KIPAPA

Toka Roma ya Kipagani Kwenda Roma ya Kipapa

Katika  karne  ile  ya  sita  upapa  ulikuwa  umejiimarisha sana.   Kiti  chake  cha  enzi  kilikuwa  katika  mji  ule  wa  dola [Roma],  na  Askofu  wa  Roma  [Papa]  akatangazwa  kuwa  ndiye kichwa  cha  kanisa  lote.   Upagani  ukaupa  upapa  nafasi  yake [Dan.  8:12;   12:11].   Yule  Joka  [Ibilisi  na  Roma  ya  Kipagani  Ufu.  12:9,3]  alikuwa  amempa  mnyama  [mfalme  –  Dan.  7:17] “nguvu  zake  na  kiti  chake  cha  enzi,  na  uwezo  mwingi.”   Ufunuo 13:2.   Na  sasa  ikaanza  ile  miaka  1260  ya  mateso  [mauaji]  ya papa  yaliyokuwa  yametabiriwa  katika  unabii  wa  Danieli  na Ufunuo.  Danieli  7:25;  Ufunuo  13:5-7.  Wakristo wakalazimishwa  ama  kuuacha  msimamo  wao  mnyofu  na kuzikubali  sherehe  za  kipapa  pamoja  na  ibada  yake,  ama kuchomwa  moto  juu  ya  kitita  cha  kuni,  ama  kukabiliwa  na  mtu yule  akataye  vichwa  kwa  shoka.   Basi,  maneno  ya  Yesu  yakawa yametimizwa,  aliyosema:   “Nanyi  mtasalitiwa  na  wazazi  wenu, na  ndugu  zenu,  na  jamaa  zenu,  na  rafiki  zenu,  nao  watawafisha [watawaua]  baadhi  yenu.   Nanyi  mtachukiwa  na  watu  wote  kwa ajili  ya  jina  langu.”   Luka  21:16,17.   Mateso  yakaanzishwa  rasmi dhidi  ya  wale  waliokuwa  waaminifu  kwa  ukali  sana  kuliko wakati  wo  wote  uliopita,  na  dunia  hii  ikawa  ni  uwanja  mkubwa wa  vita.   Kwa  mamia  ya  miaka  Kanisa  la  Kristo  likapata kimbilio  lake  katika  maeneo  ya  upweke  na  ya  siri.   Nabii  yule asema  hivi:   “Yule  mwanamke  [Kanisa  la  Kristo  la  Kweli] akakimbilia  nyikani,  ambapo  ana  mahali  palipotengenezwa  na Mungu,  ili  wamlishe  huko  kwa  muda  wa  siku  [miaka  –  Eze.  4:6] elfu na mia mbili na sitini.”  Ufunuo 12:6ZAMA ZA GIZA ZAANZA Kule  kujipatia  mamlaka  yake  lile  Kanisa  la  Roma  ndio mwanzo  wa  Zama  za  Giza.   Kadiri  uwezo  wake  ulivyozidi kuongezeka,  ndivyo  giza  [yaani,  ujinga  wa  kutoijua  Biblia, Sayansi  na  Teknolojia]  lilivyozidi  kuwa  nene.   Imani ikahamishwa  kutoka  kwa  Kristo,  aliye  msingi  wa  kweli,  kwenda kwa  papa  wa  Roma.   Badala  ya  kumtegemea  Mwana  wa  Mungu kwa  msamaha  wa  dhambi  na  wokovu  ule  wa  milele,  watu wakamtazama  papa,  na  makasisi  (mapadre)  na  maaskofu  ambao alikuwa  amewakabidhi  mamlaka.   Wakafundishwa  ya  kwamba papa  alikuwa  ndiye  mpatanishi  wao  wa  kibinadamu  na  ya kwamba  hakuna  hata  mmoja  ambaye  angeweza  kumwendea Mungu  isipokuwa  kwa  kupitia  kwake,  na  kwa  ajili  hiyo  yeye alipaswa  kupewa  utii  bila  swali  lo  lote.   Kwenda  kinyume  na matakwa  yake  ilikuwa  ni  sababu  ya  kutosha  ya  kutolewa  adhabu kali  sana  juu  ya  miili  na  roho  za  wale  wahalifu.   Kwa  njia  hiyo, mawazo  ya  watu  yakageuziwa  mbali  na  Mungu  na  kuelekezwa kwa  wanadamu  wawezao  kukosa,  kupotoka,  na  wakatili,  naam, zaidi  sana,  kwa  yule  mkuu  wa  giza  mwenyewe  [Shetani], ambaye  alitumia  uwezo  wake  kupitia  kwa  watu  wale.   Dhambi ikafichwa  katika  vazi  la  utakatifu.   Maandiko  yanapozuiwa kusomwa  na  watu,  na  mwanadamu  anapokuja  kujiona mwenyewe  kuwa  ni  mkubwa  kuliko  wote,  hapo  ndipo tunapohitaji  tu  kutazamia  kuona  hila,  udanganyifu,  na  uovu unaoishusha  hadhi  ya  mwanadamu.   Katika  kuzitukuza  sheria  za wanadamu  na  mapokeo  ukaonekana  ufisadi  ambao  hutokea daima  wakati  Sheria  ya  Mungu  [Amri  Kumi]  inapowekwa kando.Siku za Hatari Kubwa Kristo.  Zile  zilikuwa  ni  siku  za  hatari  kubwa  kwa  Kanisa  lake Waaminifu  walioibeba  bendera  yake  walikuwa  ni wachache  kweli  kweli.   Ingawa  ile  kweli  haikuachwa  bila kuwapo  mashahidi,  hata  hivyo,  wakati  fulani  ilionekana  kana kwamba  mafundisho  yale  ya  uongo  na  ushirikina  yalikuwa yameenea  kote,  na  dini  ile  ya  kweli  ilionekana  kana  kwamba ingeweza  kufutiliwa  mbali  duniani  kote.   Injili  ikawa imesahauliwa,  lakini  mitindo  ya  dini  ikaongezeka,  na  watu wakawa  wamelemewa  na  mizigo  mizito  waliyotwishwa  yenye masharti makali. Wakafundishwa  sio  tu  kumtazama  papa  kama  ndiye mpatanishi  wao,  bali  kutegemea  matendo  yao  wenyewe  ili kuweza  kulipa  fidia  ya  dhambi  zao.   Safari  ndefu  za  taabu kwenda  kuzuru  patakatifu,  kutenda  matendo  ya  kitubio,  kuabudu mifupa  ya  watakatifu  waliokufa  zamani,  kujenga  makanisa, kujenga  makaburi  ya  watakatifu,  na  altare  [madhabahu],  kulipa fedha  nyingi  kwa  kanisa   -   mambo  hayo  pamoja  na  matendo mengine  yanayofanana  na  hayo  yaliamriwa  ili  kuituliza ghadhabu  ya  Mungu  au  kupata  upendeleo  wake,  kana  kwamba Mungu  alikuwa  kama  wanadamu,  kuweza  kukasirishwa  kwa mambo  madogo  sana  yasiyo  na  maana,  au  kutulizwa  kwa kupewa zawadi au kwa maungamo (kitubio)! Giza  lile  likaonekana  kana  kwamba  lilikuwa likiongezeka  kuwa  nene  zaidi.   Ibada  ya  sanamu  ikawa  ni  la  kawaida  kwa  watu  wengi.   Mishumaa  ikawashwa  mbele  ya sanamu  zile  na  sala  zikatolewa  kwa  sanamu  zile.   Desturi  zile  za kipuuzi  kabisa  na  za  kishirikina,  hata  akili  zao  zenyewe zikaonekana  kana  kwamba  zimepoteza  uwezo  wake  wa kujitawala.   Wakati  wale  makasisi  (mapadre)  na  maaskofu wenyewe  walikuwa  wanapenda  anasa,  uasherati,  na  ufisadi, iliweza  kutazamiwa  tu  kwamba,  watu  wale  waliowategemea kwa  uongozi  wao,  nao  wangeweza  kuzama  katika  ujinga  na uovu wao.Papa yule Mwenye Majivuno Hatua  nyingine  katika  dhana  za  kipapa  ilichukuliwa katika  karne  ile  ya  kumi  na  moja  wakati  Papa  Gregori  wa  Saba alipotangaza  ukamilifu  wa  Kanisa  la  Roma.   Miongoni  mwa mawazo  yake  aliyotoa  lilikuwapo  wazo  moja  lililosema  kwamba kanisa  lile  [la  Roma]  lilikuwa  halijapata  kukosea  kamwe kulingana  na  Maandiko.   Lakini  ushuhuda  wa  Maandiko  hayo haukuambaatana  na  lile  dai  lake.   Papa  yule  mwenye  majivuno mengi  alidai  pia  kwamba  anao  uwezo  wa  kuwaondoa  wafalme katika  kiti  chao  cha  enzi,  kisha  akatangaza  kwamba  hakuna hukumu  yo  yote  aliyoitoa  yeye  ambayo  ingeweza  kubatilishwa [kugeuzwa]  na  mtu  ye  yote,  ila  kwamba  yeye  ndiye  alikuwa  na haki ya kuyabatilisha [kuyageuza] maamuzi ya wengine wote. Ni  tofauti  kubwa  ya  kushangaza  mno  jinsi  gani  kati  ya kiburi  kile  kilichojaa  uonevu  cha  papa  yule  mwenye  majivuno mengi  ukilinganisha  na  upole  na  unyenyekevu  wa  moyo aliokuwa  nao  Kristo,  ambaye  anajiwakilisha  mwenyewe  kama mmoja  anayebisha  katika  mlango  wa  moyo  akiomba  kuingia ndani,  ili  apate  kuingia  humo  na  kuleta  msamaha  na  amani,  na ambaye  aliwafundisha  wanafunzi  wake,  akasema:   “Na  mtu  ye yote  anayetaka  kuwa  wa  kwanza  kwenu  na  awe  mtumwa  wenu.” Mathayo 20:27.Giza Lazidi Kuwa Nene Karne  zile  zilipozidi  kusonga  mbele  zilishuhudia ongezeko  la  daima  la  uongo  katika  mafundisho  ya  dini yaliyotolewa  kutoka  Roma.   Hata  kabla  ya  kuanzishwa  kwa upapa  mafundisho  ya  wanafalsafa  wale  makafiri  yalikuwa yamezingatiwa,  nayo  yalitoa  mvuto  wake  ndani  ya  kanisa. Wengi  waliodai  kwamba  wameongoka  walikuwa  bado wanazing'ang'ania  itikadi  za  falsafa  yao  ya  kipagani,  na  si kwamba  tu  waliendelea  kujifunza  falsafa  hiyo  wao  wenyewe, bali  waliwashurutisha  wengine  kuipokea  kama  njia  ya  kueneza mvuto  wao  miongoni  mwa  makafiri  wale.   Makosa  mazito yakaingizwa  kwa  njia  hiyo  katika  imani  ya  Kikristo. Lililojitokeza  sana  katika  hayo  ni  ile  imani  kwamba mwanadamu  ana  roho  isiyokufa,  na  ya  kwamba,  akifa  bado anaendelea  kuwa  na  fahamu  zake.   Fundisho  hilo  la  dini likaweka  msingi  ambao  juu  yake  Roma  ilianzisha  sala  kwa  ajili ya  watakatifu  waliokufa  na  ibada  ya  Bikira  Maria.   Kutokana  na fundisho  hilo  pia  ukazuka  uzushi  uliosema  kwamba  wale  ambao hatimaye  hawataweza  kutubu  wataendelea  kuteswa  motoni milele  hata  milele,  fundisho  ambalo  liliingizwa  katika  imani  ya kipapa.Ndipo  njia  ikawa  imetayarishwa  ya  kuingizwa  [kanisani] mavumbuzi  mengine  ya  kipagani  ambayo  Roma  iliyaita  kwa jina  la  'Toharani'  (purgatory),  nao  wakalitumia  fundisho  hilo kuwatisha  makundi  ya  watu  wale  waliokuwa  wajinga  na washirikina.   Kwa  uzushi  wao  huo,  wanathibitisha  kwamba  pako mahali  pa  mateso,  ambapo  roho  za  wale  wasiostahili  adhabu  ya milele  zinapaswa  kuadhibiwa  kwa  ajili  ya  dhambi  zao,  na  ya kwamba,  kutoka  hapo,  zinapowekwa  huru  mbali  na  uchafu wake, roho hizo huingizwa mbinguni.
Mtazamo wa Kifedha Bado  ikawapo  haja  ya  kubuni  uongo  mwingine  ili kuiwezesha  Roma  kunufaika  kutokana  na  hofu  hiyo  na  maovu ya  wafuasi  wake.   Uongo  huo  uliwezekana  kwa  fundisho  lao  la indulgensia  [ondoleo  la  dhambi].   Ondoleo  kamili  la  dhambi, zilizopita,  za  sasa,  na  za  baadaye,  na  kuachiliwa  ili  mtu  asiweze kupatikana  na  maumivu  yote  pamoja  na  adhabu  anazostahili [toharani],  wakawa  wameahidiwa  kupewa  wale  wote  ambao wangejiandikisha  katika  vita  vya  papa  ili  kupanua  mipaka  ya utawala  wake  wa  kidunia,  ili  kuwaadhibu  maadui  zake,  au kuwaangamiza  kabisa  wale  ambao  wangethubutu  kuupinga  ukuu wake  usio  na  kifani.   Watu  walifundishwa  pia  kwamba  kwa kulipa  fedha  kwa  kanisa  wangeweza  kujiweka  huru  mbali  na dhambi,  na  pia  kuzifungua  roho  za  marafiki  zao  waliokufa zilizokuwa  zimefungiwa  katika  moto  ule  wa  mateso.   Kwa  njia kama  hizo  Roma  ilijaza  makasha  yake  kwa  fedha  na  kuendeleza ufahari,  anasa,  na  uovu  wa  wale  wawakilishi  wanafiki  wa  yeye [Kristo], ambaye hakuwa na mahali pa kulaza kichwa chake. "Papa  si  mwakilishi  tu  wa  Yesu Kristo,  bali  yeye  ndiye  Yesu Kristo,  aliyejificha  katika  vazi  la mwili." The Catholic National, Julai 1895.Muumbaji Aumbwa Agizo  la  Maandiko  kuhusu  Meza  ya  Bwana  lilikuwa limeondolewa  na  mahali  pake  ikawekwa  ibada  ya  sanamu  ya Misa.   Makasisi  (mapadre)  wa  kikatoliki,  kwaa  kutamka  maneno fulani  ya  kidini  yasiyo  na  maana,  wakajifanya  kuwa  wanaweza kuugeuza  mkate  wa  kawaida  na  divai  kuwa  "mwili  na  damu [halisi]  ya  Kristo."   -   Kadinali  Wiseman,   The  Real  Presence  of the  Body  and  Blood  of  Our  Lord  Jesus  Christ  in  the  Blessed Eucharist,  Provede  From  Scripture,  hotuba  ya  8,  Sehemu  ya  3, aya  ya  26.   Kwa  kiburi  chao  cha  makusudi  kabisa  kilichojaa makufuru,  walidai  waziwazi  kwamba  wanao  uwezo  wa kumwumba  Mungu,  Muumbaji  wa  vitu  vyote.   Wakristo walitakiwa,  kwa  tishio  la  kifo,  kukiri  imani  yao  katika  uzushi huo  wa  kutisha  unaoitukanisha  Mbingu.   Watu  wengi  waliokataa walitupwa motoni.
Mamilioni ya Wafiadini Katika  karne  ile  ya  kumi  na  tatu  kilianzishwa  chombo cha  papa  cha  kutisha  mno,   -   yaani,  ile  Inkwizisheni  [Mahakama ya  Kanisa  Katoliki  ya  kukomesha  uasi].   Mkuu  yule  wa  giza alifanya  kazi  yake  pamoja  na  viongozi  wa  utawala  huo  msonge wa  kipapa.   Katika  mabaraza  yao  ya  siri  Shetani  na  malaika  zake waliyatawala  mawazo  ya  watu  wale  waovu,  ijapokuwa  alikuwa haonekani  kwa  macho,  malaika  wa  Mungu  alikuwa  amesimama katikati  yao,  akichukua  kumbukumbu  ya  kutisha  ya  amri  zao zilizojaa  uovu  na  kuandika  historia  ya  matendo  yao  ya  kutisha mno  kuweza  kuonwa  kwa  macho  ya  kibinadamu.   "Babeli Mkuu"  [Roma]  alikuwa  "amelewa  na  damu  ya  watakatifu." Miili  ya  mamilioni  ya  wafiadini  iliyokuwa  imeharibiwa  vibaya ikamlilia Mungu ili apate kulipiza kisasi kwa mamlaka hiyo asi. "Papa  Yohane  Paulo  II  aliomba  msamaha  kwa  ajili ya  vita  iliyopiganwa  kule  Ulaya  kati  ya  Wakatoliki na  Waprotestanti  katika  kipindi  kile  cha  Upingaji wa  Matengenezo  ya  Kanisa  Counter-Reformation)." U. S. News and World Report,  Julai  3,  1995.Taarifa  za  habari  hii  pamoja  na  habari  nyingine zinazofanana  na  hii  ni kukiri  uwajibikaji  kwa mauaji  ya  mamilioni  ya  wafiadini  katika  kipindi  kile cha   za  Giza  kwa  kutumia  njia  ya  mzunguko.   Biblia inatabiri  kwamba  chini  ya  hali  zile  za  dhiki  zilizo mbele  yetu  hivi  sasa,  Upapa  na  wale  wanaouunga mkono  watatumia  tena  nguvu  za  dola  (serikali) kuwadhibiti  wale  wasiokubaliana  na  mafundisho yao  ya  dini. ******* "Kwa  kukiri  imani  iliyo  kinyume  na    Kanisa  la Roma,  historia  inaweka  kumbukumbu  ya  wafiadini zaidi  ya  watu  milioni  mia  moja."   Brief  Bible Readings,  ukurasa 16. "Tarehe  24  Agosti,  1527,  Wakatoliki  wa  Roma  kule Ufaransa,  kwa  mpango  uliokuwa  umepangwa mapema  chini  ya  uongozi  wa  Majesuti,  waliwaua Waprotestanti  70,000  Katika  kipindi  cha  miezi miwili.   Papa  alishangilia  sana  kusikia  matokeo hayo yaliyofaulu."   Western Watchman,  Novemba, 21, 1912, (La Kikatoliki).
"Kwamba  hilo  Kanisa  la  Roma  limemwaga  damu nyingi  sana  isiyo  na  hatia  kuliko  taasisi  nyingine  yo yote  iliyopata  kuwako  miongoni  mwa  binadamu, jambo  hilo  halitaweza  kutiliwa  mashaka  yo  yote  na Mprotestanti  ye  yote  aliye  na  ujuzi  wa  kutosha  wa Historia….   Haiwezekani  kabisa  kuwa  na  dhana kamili  ya  idadi  kubwa  ya  wahanga  wake  waliouawa ."   W.  E.  H.  Lecky,  History  of  the  Rise  and  Influence of  the  Spirit  of  Rationalism  in  Europe,  gombo  la  2, ukurasa 32, toleo la 1910. "Inakadiriwa   …  wastani  wa  mauaji  ya  kidini  ya watu  40,000  kwa  kila     mwaka  wa  kuwako  kwa Upapa."   John  Dowling,  The  History  of  Romanism, ukurasa  541-542.   [Upapa  ulitawala  miaka  1260 kuanzia  538  B.K.  hadi  1798  B.K.   Kwa  hiyo  makadirio ya  chini  kabisa  ya  wafiadini  waliouawa  na  Kanisa  la Roma ni 1260 x 40,000 = 50,400,000.]


Newest
Previous
Next Post »

1 comments:

Click here for comments
Unknown
admin
18 April 2024 at 13:13 ×

ndugu hizo mada unaweza kunitumia kwa WhatsApp ili niweze kusoma vzr

Congrats bro Unknown you got PERTAMAX...! hehehehe...
Reply
avatar