CHIMBUKO LA DHAMBI

Chimbuko la Dhambi Katika  mawazo  ya  watu  wengi  chimbuko  la  uovu  na sababu  ya  kuwapo  kwake  ni  chanzo  cha  utata  mkubwa  sana kwao.   Wanaona  matendo  mabaya,  pamoja  na  matokeo  yake  ya kutisha  yaletayo  misiba  na  maangamizi,  nao  huuliza  kwamba mambo  hayo  yote  yanawezaje  kuwapo  chini  ya  utawala  wa  yule Mmoja aliye na hekima, uweza, na upendo usio na kikomo. Ni  jambo  lisilowezekana  kabisa  kueleza  chimbuko  hilo la  dhambi  kwa  kiasi  cha  kuweza  kutoa  sababu  ya  kuwapo kwake.   Lakini  kinaweza  kufahamika  kiasi  cha  kutosheleza  kwa mambo  haya  mawili,  chimbuko  la  dhambi  na  kuondolewa kwake  hatimaye,  ili  kudhihirisha  kwa  ukamilifu  haki  na  fadhili zake  Mungu  katika  kuushughulikia  kwake  kote  uovu  huo. Dhambi  ni  kitu  kinachojiingiza  chenyewe,  kuwako  kwake hakuna  sababu  iwezayo  kutolewa.   Kama  udhuru  wo  wote ungeweza  kupatikana  wa  kuwako  kwa  dhambi  hiyo,  au  sababu yo  yote  ingeweza  kutolewa  kwa  kuwako  kwake,  basi,  ingekoma kuwa  dhambi.   Maana  ya  dhambi  tuliyo  nayo  peke  yake  ni  ile iliyotolewa  katika  Neno  la  Mungu;   yaani,  [dhambi]  ni uvunjaji wa Sheria  [Amri Kumi - 1 Yohana 3:4, AJKK].Upendo wa Mungu dhidi ya Kiburi Sheria  ile  ya  upendo  [Amri  Kumi  -  Mt.  22:35-40;   Rum. 13:8-10;   Yak.  2:10-12]  ikiwa  ndiyo  msingi  wa  Serikali  ya Mungu,  basi,  kule  kuafikiana  kabisa  na  kanuni  zake  za  haki lilikuwa  ndilo  tegemeo  la  furaha  ya  viumbe  vyote vilivyoumbwa.   Mungu  anataka  huduma  ya  upendo  toka  kwa viumbe  vyake  vyote   -   yaani,  ibada  ile  itokanayo  na  kuithamini tabia  yake  kwa  kutumia  akili  zetu.   Haufurahii  utii  unaotolewa kwake  kwa  kujilazimisha,  tena  yeye  huwapa  wote  uhuru  wa kufanya  wapendavyo,  ili  waweze  kumpa  huduma  yao  ya  hiari. Lakini  alikuwako  mmoja  aliyechagua  kuutumia  vibaya  uhuru wake.   Dhambi  ilianzishwa  na  huyo,  ambaye,  akiwa  wa  pili toka  kwa  Kristo,  alikuwa  amepewa  heshima  kubwa  sana,  naye alikuwa  amesimama  mahali  pa  juu  sana  pa  mamlaka  na  utukufu miongoni  mwa  wakazi  wote  wa  mbinguni.   Kabla  ya  anguko lake,  Lusifa  [Lucifer  =  Nyota  ya  Alfajiri   -   Isa.  14:12,  KJV] alikuwa  Kerubi  afunikaye  wa  kwanza,  mtakatifu,  na  asiye  na waa.  Angalia Ezekieli 28:12-15. Lusifa  angeweza  kubakia  katika  upendeleo  wa  Mungu, akiwa  anapendwa  na  kuheshimiwa  na  jeshi  lote  la  malaika, akitumia  uwezo  wake  mkuu  kuwaletea  furaha  wengine  na kumtukuza  Muumbaji  wake.   Lakini,  asema  hivi  huyo  nabii, "Moyo  wako  uliinuka  kwa  sababu  ya  uzuri  wako;   umeiharibu hekima  yako  kwa  sababu  ya  mwangaza  wako."   Ezekieli  28:17. Kidogo  kidogo,  Lusifa  akaanza  kuingiwa  na  tamaa  ya  kujikweza mwenyewe.   "Nawe  ulisema   …   Nitapaa  kupita  vimo  vya mawingu,  Nitafanana  na  Yeye  Aliye  Juu."   Isaya  14:13,14. Badala  ya  yeye  kumfanya  Mungu  aonekane  kuwa  ndiye  kuliko  wote  katika  mapenzi  na  utiifu  wa  viumbe  vyake,  ilikuwa ni  jitihada  yake  Lusifa  kuwashawishi  watoe  huduma  yao  pamoja na  utii  wao  kwake  yeye  mwenyewe.   Naye  akiwa  anatamani sana  heshima  ile  ambayo  Baba  wa  milele  alikuwa  amempa Mwanawe,  mkuu  huyo  wa  malaika  akataka  sana  kujinyakulia mamlaka  yale  ambayo  ilikuwa  ni  haki  yake  Kristo  peke  yake kuyatumia. Mwana  wa  Mungu  alikuwa  ndiye  Mfalme  wa  mbinguni aliyetambulikana  hivyo,  akiwa  na  uweza  na  mamlaka  kama Baba  yake.   Katika  mashauri  ya  Mungu,  Kristo  alishiriki, ambapo  Lusifa  hakuruhusiwa  hivyo  kuingia  katika  makusudi  ya Mungu.   "Kwa  nini  Kristo  awe  mkuu  kuliko  wote"?   akauliza yule  malaika  mwenye  uwezo  mwingi,   "Kwa  nini  yeye anaheshimiwa kuliko mimi Lusifa?"Ajivika Usiri Shetani  alikuwa  amepewa  heshima  kubwa  sana,  na matendo  yake  yote  yalikuwa  na  usiri,  hata  ikawa  vigumu  [kwa Mungu]  kuwafunulia  malaika  wale  hali  halisi  ya  kazi  yake. Mpaka  hapo  itakapofikia  ukamilifu  wake,  dhambi isingalionekana  kuwa  ni  kitu  kibaya  kama  vile  ilivyo.   Mpaka wakati  ule  ilikuwa  haina  nafasi  yo  yote  katika  malimwengu  ya Mungu,  wala  viumbe  wale  watakatifu  hawakuwa  na  wazo  lo  lote kuhusu  hali  yake  halisi,  wala  ubaya  wake.   Hawakuweza kutambua  athari  zake  zitakazotokea  kwa  kitendo  cha  kuiweka kando  Sheria  ya  Mungu  [Amri  Kumi].   Katika  kuishughulikia dhambi,  Mungu  angeweza  kutumia  haki  na  kweli  tupu.   Shetani angeweza  kutumia  kile  ambacho  Mungu  asingeweza  kutumia   yaani,  kujipendekeza  na  udanganyifu.  Hali  ile  ya kutokuelewana  iliyosababishwa  na  mwenendo  wake  kule mbinguni,  Shetani  akailaumu  Sheria  [Amri  Kumi]  na  Serikali  ya Mungu  [kuwa  ndicho  chanzo  chake].   Akatangaza  kwamba maovu  yote  yalikuwa  ni  matokeo  ya  utawala  wa  Mungu. Akadai  kwamba  lilikuwa  ni  lengo  lake  kuziboresha  Sheria  za Yehova.   Kwa  ajili  hiyo,  ilikuwa  ni  lazima  kwamba  aonyeshe sura  ya  madai  yake,  na  kuonyesha  utendaji  wa  mabadiliko  yake aliyokuwa  amependekeza  yafanyike  katika  Sheria  ile  ya  Mungu [Amri  Kumi].   Kazi  yake  ni  lazima  imhukumu  mwenyewe. Tangu  mwanzo  Shetani  alikuwa  amedai  kwamba  alikuwa hajafanya  maasi  yo  yote.  Ni  lazima  apewe  muda  wa  kujifunua mwenyewe  kwa  kazi  zake  za  uovu.   Ulimwengu  wote  unapaswa kumwona laghai huyo akiwa amefuchuliwaRoho Ile Ile Roho  ile  ile  iliyochochea  maasi  kule  mbinguni  bado inaendelea  kuchochea  maasi  hapa  duniani.   Shetani  ameendelea kushughulika  na  wanadamu  kwa  kutumia  mbinu  yake  ile  ile aliyoitumia  kwa  wale  malaika.   Kwa  njia  ile  ile  ya  kuieleza vibaya  tabia  ya  Mungu  kama  vile  alivyofanya  mbinguni, alipomfanya  [Mungu]  afikiriwe  kuwa  ni  mkali  tena  ni  dhalimu, Shetani  alimshawishi  mwanadamu  kutenda  dhambi.   Na  baada ya  kufanikiwa  mpaka  pale,  akatangaza  kwamba  vizuio  vyote  vya Mungu  ambavyo  vilikuwa  si  vya  haki  ndivyo  vilivyosababisha mwanadamu  kuanguka  dhambini,  kama  vile  vilivyomfanya  yeye kuangukia  katika  maasi  yale.   Mungu  alitoa  ushahidi  wa  upendo wake  kwa  kumtoa  Mwanawe  pekee  kufa  kwa  ajili  ya  wanadamu walioanguka  [dhambini   -   Yn.  3:16].   Katika  upatanisho  huo tabia  ya  Mungu  imedhihirika.   Hoja  ile  yenye  nguvu  ya  msalaba hudhihirisha  kwa  malimwengu  yote  kwamba,  kwa  vyo  vyote vile,  Serikali  ya  Mungu  isingestahili  kutupiwa  lawama  yo  yote kutokana na njia ile ya dhambi aliyoichagua Lusifa.
Kama tulivyoona chanzo cha dhambi ni kujiinua kwa yule aliyekuwa malaika mkuu Lucifer ambae hatimaye alishindwa vita iliyotokea mbinguni akatupwa hapa duniani akaitawala dunia yote ndipo  Yesu kristo akaja kutufilia msalabani ,Mipango wa shetani daima ni uharibifu wa kila  namna akiri zetu sio jambo la kushangaza kwa leo jinsi alivyoteka wanadamu kwa njia hata ya mitandao akiri zimefungwa kutoka katika kutafakari neno la Mungu, tumshukuru Mungu kwa kukupatia huu Ujumbe jitenge MBALI na uovu wa ibilisi ,maadamu tu NEEMA ingalipo
Karibu kwa somo linalofuata.
Previous
Next Post »