MFALME WA AMANI ANAKUJA UPESI

MFALME WA AMANI ANAKUJA UPESI SANA
(SOMA  DANIELI  2  YOTE)
Mpendwa nnakukaribisha katika mfululizo wa masomo ya unabii kutoka katika kitabu cha Daniel ,kumbuka anaheri asomaye na wale wanaosikia neno la Mungu ,hivyo hautajuta kujifunza masomo haya Bwana akubariki unapofuatilia kupitia ukurasa huu .
Katika historia ya ulimwengu huu
Hakuna mwanadamu ye yote awezaye kutabiri kwa hakika  mambo  yatakayokuja baadaye  kwa  hekima  au  maarifa yake  mwenyewe.   Wanajimu [wanaobashiri kwa  kuangalia nyota], wachawi  wanaotazama  bao,  wasoma  viganja,  hata  wana  sayansi  wanabahatisha  tu, hawawezi  kujua kwa  hakika  mambo ya zamani au  mambo yanayokuja  mbele hebu na tusome haya mafungu twende kwa wamoja (Dan.2:27,28; Isa.  42:8,9;   46:9,10;  41:21-24;  8:19;  Yak.  4:13-16).   Ni  Mungu  peke  yake  anayejua mambo ya zamani  na  yale  yajayo,  naye  anatuambia  kabla  hayajatokea.    Tangu  dhambi iingie duniani  mawasiliano  ya  moja  kwa  moja  na  Mungu  yalikatika;  anawasiliana  nasi kupitia  kwa  manabii  anaowachagua  mwenyewe  (Isa.59:2;   Hes.  12:6).   Matukio  yote makubwa  yanayoleta  maafa  kwa  wanadamu  anawajulisha  manabii  wake  (Amosi  3:7). Kuhusu  Gharika  alimjulisha  Nuhu;   kuangamizwa  kwa  Ninawi  alimjulisha  Yona; kuangamizwa kwa Sodoma na Gomora alimjulisha Ibrahimu.   Mbele  yetu  kuna  mapigo saba  hebu soma hilifungu(Ufunuo 16)  ambayo  yatawaathiri sana  wanadamu.   Kabla  hayajaja alimjulisha Yohana kisiwani  Patmo.   Maafa  yaliyotiishiwa  yanaweza  kuepukwa  kama  watu  wanaohusika watatubu na kuacha dhambi zao (Yer. 18:7-10;  Yona 3:1-10). Tukiwakataa manabii wanaotumwa na Mungu hatutafanikiwa katika safari yetu ya mbinguni  (2  Nya.  20:20).    Japo  vitabu  vya  Biblia  vilifungwa (Vitabu 66  -  Agano la Kale  39;  Agano Jipya 27),  bado  manabii  wataendelea  kutumwa  na  Mungu  kulionya  kanisa  lake (Yoeli  2:28-31;   Efe.4:11-14).   Kwa  kuwa  wako  manabii  wa  uongo,  basi,  yatupasa kuwapima.  Viko vipimo vinne ambayo nabii ni lazima atimize vyote kuweza kukubalika kama nabii  wa kweli  wa  Mungu   -----  

hebu soma haya mafungu

1.  Yer.  28:9;   Kum.  13:1-5;  
2.  Isa.  8:20 [Kut.20:3-17];  
3.   Mt.  7:20;    
4.    1  Yoh.  4:1-3).  
 Kupitia haya mafungu ndipo Unaweza kumtambua nabii wa kweli ,lakini asipoenda Sawa na neno hili huyo sio nabii wa kweli ,je, umeweza kutofautisha ?.

Kumbuka kuwa  Unabii  na  Historia  vinakwenda  bega  kwa  bega (Yohana  14:29).   Tafsiri  sahihi ya unabii  itaungwa mkono  na  mafungu  ya  Biblia  na Historia (Isa. 28:10;  2  Pet.  1:19-21).  
 Unabii  hautafsiriwi  kama  mtu  apendavyo  au  kama  kanisa fulani lipendavyo .
je , wewe ndoto unazichukuliaje ?

Ndoto aliyoota mfalme iliyomfadhaisha sana ilihusu Falme Kuu Nne zilizotawala dunia na Falme zilizofuata hadi kuja kwa Yesu  Kristo kuja kusimamisha ufalme wake wa milele.  Tafsiri ni hii:

I. UFALME WA BABELI
Ulitokea miaka ya(606-538 au 605-539 K.K.).
Umewakilishwa na
Kichwa  cha dhahabu  
(Dan. 2:37-38).   Historia  inaunga mkono.
II. UFALME WA WAMEDI NA WAAJEMI
Ulitokea kati ya mwaka (538-331 au 539-331 K.K.).
Uliuangusha Ufalme wa  Babeli  (Dan. 5:25-31).   Unawakilishwa na  Kifua  na  Mikono ya Fedha  (Dan. 2:32a,39a).  
Historia inaunga mkono.  Miaka ni ya kukadiria tu.
 III. UFALME WA WAYUNANI
(331-168 K.K.)

Ufalme wa Wamedi na Waajemi ulitabiriwa  kuwa utaangushwa  na Wayunani  (Dan. 8:4-7,20-21;  11:13). 
  Ufalme  wa  Wayunani  (Wagiriki)  unawakilishwa  na  Tumbo  na Viuno vya Shaba  (Dan. 2:32b,39b).  Historia inaunga mkono.
 IV. UFALME WA WARUMI (168 K.K. - 476 B.K.).
 Ufalme wa Warumi unawakilishwa na  Miguu ya Chuma.   Biblia  inaielezea  vizuri Dola ya Warumi kuwa ilikuwa  inazivunja-vunja  falme zile nyingine  kama chuma.  Danieli hakujulishwa jina la Dola hii.  Lakini  historia  inathibitisha  kuwa  Warumi  waliwashinda Wayunani  mwaka  ule  wa  168  K.K.    Wakati  Kristo  anazaliwa  Dola  hiyo  ilikuwa  bado inatawala  dunia  pamoja  na  Palestina  chini  ya  Kaisari  Augusto  (Luka  2:1-7;  Yohana  11:48)

UFALME WA PAPA (538-1798 B.K.)

Ulitokea katika mabaki ya Dola ya Warumi baada ya kuangushwa na makabila ya [kipagani]  ya  Ulaya Kaskazini  mwaka  wa  476  B.K.  Unawakilishwa  na  Nyayo za miguu  (Dan.2:33b,41a).    Udongo  unawakilisha  kanisa au watu  wa Mungu (Isa.64:8;  Yer. 18:6).   Chuma  kinawakilisha  serikali.   Hivyo  kuchanganyika  kwa  udongo  na  chuma  ni muungano  wa  dini  na  serikali  chini  ya  kiongozi  mmoja  wa  kidini  wa  Roma.    Historia inathibitisha  kwamba  ufalme  huu  uliinuka  katika  mabaki  ya  Dola  ya  Warumi  baada  ya kuangushwa na kutawala dunia kuanzia 538 B.K.  Huu ni Utawala wa Papa au Upapa.
VI. FALME KUMI ZA ULAYA MAGHARIBI (476-MAREJEO YA KRISTO)
Falme kumi za  Ulaya Magharibi  zinawakilishwa  na  Vidole  Kumi  Vya  Nyayo  (Dan. 2:42).   Falme  hizo  ni  Uingereza,  Ufaransa,  Ujerumani,  Uswisi  (Switzerland),  Ureno, Hispania,  Italia,  Waheruli  (Heruli)*,  Wavandali  (Vandals)*,  na  Waostrogothi (Ostrogoths)*.    Falme  tatu  za  mwisho huwezi  kuziona katika  ramani ya siku  hizi.  Habari zake zitatolewa  katika  somo  la Danieli  7.  Mataifa  hayo  10 yalikuwa  makoloni  ya  Warumi. Rumi  ilipoanguka  mwaka  476  yakawa  yamejikomboa  na  kuwa  huru.    Baadaye yalipoipokea  dini  ya  Katoliki  kwa  nguvu  yakajikuta  yametawaliwa  na  Papa  aliyejiita Mfalme wa wafalme kuanzia mwaka 538 B.K.
VII. UFALME WA MILELE WA KRISTO (MAREJEO YAKE HADI MILELE) Ufalme  huo  unawakilishwa  na  Jiwe  lililochongwa  bila  kazi  ya  mikono (Dan.2:34,35,44,45).  Jiwe hilo ni Kristo (Luka 20:17,18;  Mt.  21:42,44;    Mdo.  4:10-12). Huyo  ndiye  Mfalme  wa  Amani anayekuja upesi  sana (Isa.  9:6;   Ufu.22:12).  Atakapokuja atazivunjilia mbali falme  zote  za  dunia  (Ufu.11:15;    19:11-21).   Kuna kitabu katika kanisa la waadventista wa Sabato kiitwacho Majibu kwa Mashaka Yako  somo la miaka 1000 itakayoanza  atakapokuja  Kristo  mara ya pili.  Baada ya  kupita  miaka  hiyo  1000  waovu  watafufuliwa  na  kuangamizwa  katika moto  wa  milele  pamoja  na  Shetani  na  malaika  zake  na  kuwa  majivu,  ndipo  dunia  hii iliyoharibiwa  vibaya  wakati  wa  kuja  kwake  mara  ya  pili   [Yer.  4:23-27;   Ufu.  6:14-17] itakapofanywa  kuwa  mpya  pamoja na mbingu  yake (Ufunuo Sura  ya 20; Mal.  4:1-3; Eze. 28:14-19;  Ufu. 21:1;  Zaburi Sura ya 37). Ombi  letu  la  dhati  lingekuwa  ni  hili:   "Ee  Yesu,  nikumbuke  utakapoingia  katika ufalme wako"  (Luka 23:42).  Ahadi ile ile itatolewa  kwetu  kuanzia  leo  tunapomwomba ombi hilo  kama kweli  tumedhamiria kuishi  kwa ajili  yake  hapa duniani,    "Utakuwa  pamoja nami peponi"  (Luka  23:43).    Ndugu  yangu,  kwa  nini  leo hii  uipoteze  nafasi  hii  ya thamani? Kata shauri sasa kumfanya Yesu awe Bwana na Mwokozi wako.  Itumie vizuri nafasi  ya leo  kama  yule  jambazi  pale  msalabani.   Acha  kucheza  na  dhambi.   Leo  ndiyo  siku  ya wokovu wako (2 Kor. 6:2).

YESU atakapokuja ataiangamiza dhambi kamwe haitakuwa na nafasi tena je Unajua anakuja lini ? ,toa maisha yako kwake leo ,mahala popote ulipo tafta kanisa la waadventista wa Sabato ujiunge na watu wanaomngoja kristo kwa hamu kubwa pale atakapo kuja washangilie kumlaki kwenda mbinguni ,usiangalie nani anafanya nini wewe jitoe na Mungu hatakuacha ubarikiwe unapofanya maamuzi ya kupata uzima wa milele kutoka katika mauti ya milele .

Mm mwinjilisti fredrick sylvanus nnapenda kukukaribisha tena kwa masomo yanayoendelea daima ushindi wa dhambi inawezekana tukijikabidhi kwa YESU pekee maana ndiye pekee aliyeishinda dhambi .
Ubarikiwe


Previous
Next Post »