Ninakukaribisha tena rafiki Mpendwa katika muendelezo wa kitabu cha Daniel ,leo tutaangalia jinsi ambayo Mungu amekuwa akitembea na wake waaminifu katika kila kizazi ,usishangae huenda leo anatumia pia watu kusimamia taratibu zake alizotoa ,pengine anakusudia pia kukutumia wewe cha ajabu haukuwa umegundua ,ashukuriwe Mungu kwa kuupata ujumbe huu uwe tayari kuupokea na uruhusu Mungu ajivunie kukuweka kuwa hai leo ,Karibu kwa somo
(SOMA DANIELI 3 YOTE)
Unaweza ukajiuliza maswali nini kilisababisha shetani kutupwa kutoka mbinguni hadi duniani , kumbuka kwamba
tangu mbinguni Shetani amekuwa akiipiga vita Sheria ya Mungu (Amri Kumi). Anamkasirikia vibaya sana kila mtu anayezishika Amri zote Kumi za Mungu na Imani ya Yesu (Ufu.12:17; 14:12; Kut. 20:3-17). Mtu akishika Amri tisa katika hizo kumi ni sawa na mtu ambaye hashiki hata moja; Shetani hana shida na mtu kama huyo, maana yuko upande wake; hawezi kumpiga vita hata kidogo (Yak.2:10-12). Amri Kumi ndizo zinazoonyesha dhambi, kwa maana "Dhambi ni uvunjaji wa Sheria [Amri Kumi]" (1 Yohana 3:4, AJKK; Rum. 7:7). Inachukua uvunjaji wa amri moja tu kuwa mwenye dhambi. Kwa hiyo, Mkristo ye yote, haidhuru awe nani au awe na cheo gani, anayeidharau Sheria ya Mungu iliyotolewa mlimani Sinai (Amri Kumi) yuko katika hatari kubwa ya kupoteza uzima wa milele (1 Yoh. 2:3-6; 5:1-5; Zab. 119:155). Yesu aliye kielelezo chetu na ambaye ni Mungu alishika Amri Kumi za Baba yake; nasi kama wafuasi wake yatupasa kufuata kama yeye alivyoenenda(yohana15:10). Usikubali mtu ye yote akudanganye, maana "watu wabaya na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika" (2 Tim.3:13). Hao waepuke. Angalia usijidanganye mwenyewe (Gal. 6:7,8), wala usimruhusu kipofu akuongoze kipofu mwenzake, mtatumbukia wote wawili shimoni (Mt. 15:14). Uzima wa milele una thamani kubwa kiasi kwamba mtu hawezi kukubali kuupoteza vivi hivi (Mt. 22:29). Hapa tunawakuta vijana watatu wa Kiebrania kasoro Danieli hayupo safari hii. Katika Danieli 1 tuliona jinsi vijana wale wanne walivyoshinda mtihani ule wa chakula. Kula chakula au kunywa kinywaji kinachodhuru mwili kwa makusudi mazima ni kuvunja Amri ya Sita inayosema, Usiue(Kut.20:13).
Hivyo walishinda mtihani wa Amri ya Sita. Sasa wamekabiliwa na mtihani mgumu kabisa wa Amri ya Pili inayosema, "Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia. Usivisujudie wala kuvitumikia..." (Kutoka 20:4-6). Mfalme Nebukadreza baada ya kuelezwa maana ya ndoto yake aliyoota ya sanamu kubwa katika Danieli 2 kuhusu Falme zile Kuu Nne ukiwamo na ufalme wake akafanya shingo ngumu kupingana na Mungu.
Akatengeneza sanamu kubwa ya dhahabu tupu [dhahabu iliwakilisha ufalme wa Babeli] akimaanisha kwamba ufalme wa Babeli utadumu milele. Akataka sanamu hiyo iliyowekwa katika uwanda wa Dura isujudiwe na wote waliokuwapo pale (Dan.3:1-7).
Wote wakaisujudia kasoro wale vijana watatu Waebrania ----- Shadraka, Meshaki, na Abednego. Ni ujasiri ulioje katika halaiki ile walimokuwamo viongozi wakuu wa serikali ya Babeli! Watu wa Mungu wanatakiwa kuwa na ujasiri kama huo kutetea kweli ya Mungu hata kama mbingu zinadondoka
(Rum. 8:3539; Ebr. 11:32-40; Dan. 11:33).
Mfalme alijaribu kuwasihi wafanye hivyo mara watakaposikia tena filimbi na ngoma zikipigwa. Akawatishia kuwa atawatupa katika tanuru ya moto iliyokuwa kali mara saba kuliko kawaida. Lakini wao kwa upole wakasema, "Mfalme, Ee Nebukadreza, hamna haja kujibu katika neno hili. Kama ni hivyo, Mungu wetu tunayemtumikia aweza kutuokoa na tanuru ile iwakayo moto; naye atatuokoa na mkono wako, Ee mfalme. Bali kama si hivyo, ujue, Ee mfalme, ya kuwa sisi hatukubali kuitumikia miungu yako, wala kuisujudia hiyo sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha" (Dan. 3:16-18). Ndipo mfalme akakasirika sana na kuamuru wafungwe na kutupwa na wanajeshi mashujaa ndani ya tanuru ile ya moto. Wale waliowatupa walikufa kwa ukali wa moto ule. Hatimaye wakafanikiwa kuwatupa katikati ya ile tanuru iliyowaka moto. Je! kulitokea nini?Loo! mfalme akashangaa, hatukutupa watu watatu, mbona wako wanne, na mmoja anakuwa kama mwana wa miungu [Yesu alikuwa pale kuwaokoa]. Ameahidi kuwa atakuwa pamoja na watu wake mpaka mwisho wa dahari (Mt. 28:20). Hata wakipita motoni au katika maji mengi atakuwa pale tayari kuwaokoa (Isaya 43:1,2). Alitimiza ahadi yake kwao katika tukio lile la kutisha. Wakawa wanatembea ndani ya moto bila kuungua. Walipotolewa nje ya tanuru ile "wakawaona watu hao, ya kuwa ule moto ulikuwa hauna nguvu juu ya miili yao, wala nywele za vichwa vyao hazikuteketea, wala suruali zao hazikubadilika, wala harufu ya moto haikuwapata hata kidogo" (Dan. 3:27). Bwana asifiwe!!! Ana uweza wa kuokoa kabisa! Mungu anasema, "kwa maana wao wanaoniheshimu nitawaheshimu, na wao wanaonidharau watahesabiwa kuwa si kitu" (1 Sam. 2:30). Ndugu yangu, je! utasimama imara kutetea Amri Kumi za Mungu? Mfalme akatambua kuwa "hakuna Mungu mwingine awezaye kuokoa namna hii. Kisha akawakuza [akawapandisha cheo] Shadraka, na Meshaki, na Abednego, katika wilaya ya Babeli" (Dan. 3:29,30); akawadharau wale wote walioisujudu sanamu ile na kutoa amri kuwa wakisema neno lo lote juu ya Mungu wa vijana hao watakatwa vipande vipande na nyumba zao zitafanywa jaa [la takataka]. Hiyo si dharau kubwa? Kuna thawabu katika kusimama imara kutetea kweli ya Mungu. Yusufu alifungwa gerezani kwa kukataa kuzini, yaani, kuvunja Amri ya Saba (Kut. 20:14). Matokeo yake Mungu alikuwa naye gerezani na hatimaye alitolewa na kuheshimiwa kwa kupewa cheo cha Waziri Mkuu wa Misri (Mwa.39:21-23; 41:37-44). Babeli inawakilisha nguvu za giza [Shetani] zinazopigana na Amri Kumi za Mungu. Hata Babeli Mkuu wa Ufunuo anayo tabia iyo hiyo. Shetani anaitumia Babeli kutekeleza maangamizi yake juu ya watu wa Mungu wasio na hatia. Kizazi hiki cha mwisho cha Sayansi na Teknolojia kitakabiliwa na Mtihani Mgumu kuliko yote wa Amri ya Nne ihusuyo Sabato (Kut. 20:8-11). Yohana alionyeshwa kwamba kila mtu aliye hai wakati huo atajaribiwa (Ufu. 3:10). Watakaolindwa na Kristo ni wale waliolishika neno la subira yake (Ufu.14:12) ---- "Hapa ndipo penye subira ya watakatifu, hao wazishikao Amri [Kumi] za Mungu na Imani ya Yesu".
Je! utasimama chini ya Bendera ya Imanueli iliyoandikwa maneno hayo juu [Ufu. 14:12] au chini ya Bendera ya Chapa ya Mnyama [Ufu. 13:16,17] ----- iliyoandikwa siku ya kupumzika ya kizazi kipya kijacho?
Hebu kwa neema yake Mungu na tuazimie kwamba 'hatuwezi kutenda neno lo lote kinyume cha kweli, bali kwa ajili ya kweli" (2 Kor. 13:8). Lakini kweli ni nini? Neno la Mungu ni kweli; Sheria ya Mungu (Amri Kumi) ni kweli (Yoh. 17:17; Zab. 119:142).
Neno lake na Sheria yake hudumu milele (Mt. 25:35; 1 Pet. 1:23; Luka 16:17; Zab. 119:44).
Sheria yake ni "kamilifu"; hivyo huwezi kuongeza wala kupunguza kitu katika Sheria hiyo ya Amri Kumi (Zab. 19:7; Kum. 4:2,10-13).
Ndugu Mpendwa kama tulivyoona kwa kupitia somo ,muda sio mrefu ufalme wa rumi utasimama tena na kuamuru wanadamu wote kuisujudia alama ya mnyama manayeke ni kukubali kuabudu siku ya kwanza ya Juma (jumapili) .badala ya Juma mosi ,nikama vile wale vijana waebrania wakati wakiwa babeli walikuwa wamefundishwa kumtumikia Mungu na kumcha pekee bila kukengeushwa na mafundisho mengine kama yalivyo leo ,ndugu nnakuomba ukubali kujifunza neno la Mungu kwa kuzifahamu hasa vyema amri zake kumi (KUTOKA 20:3-17.)huwezi kuelewa kwa urahisi uhusiano uliopo kati ya amri kumi na wokovu ,Karibu kwa kanisa linalofundisha amri zote kumi kanisa la waadventista wa Sabato popote ulipo waweza kulipata kama utakuwa na swali juu ya masomo haya tahadhali usisite kuuliza .
Ninakukaribisha kwa somo linalofuata ambalo nimhimu sana kwa hatima ya maisha YETU .Bwana akubariki sana .
(SOMA DANIELI 3 YOTE)
Unaweza ukajiuliza maswali nini kilisababisha shetani kutupwa kutoka mbinguni hadi duniani , kumbuka kwamba
tangu mbinguni Shetani amekuwa akiipiga vita Sheria ya Mungu (Amri Kumi). Anamkasirikia vibaya sana kila mtu anayezishika Amri zote Kumi za Mungu na Imani ya Yesu (Ufu.12:17; 14:12; Kut. 20:3-17). Mtu akishika Amri tisa katika hizo kumi ni sawa na mtu ambaye hashiki hata moja; Shetani hana shida na mtu kama huyo, maana yuko upande wake; hawezi kumpiga vita hata kidogo (Yak.2:10-12). Amri Kumi ndizo zinazoonyesha dhambi, kwa maana "Dhambi ni uvunjaji wa Sheria [Amri Kumi]" (1 Yohana 3:4, AJKK; Rum. 7:7). Inachukua uvunjaji wa amri moja tu kuwa mwenye dhambi. Kwa hiyo, Mkristo ye yote, haidhuru awe nani au awe na cheo gani, anayeidharau Sheria ya Mungu iliyotolewa mlimani Sinai (Amri Kumi) yuko katika hatari kubwa ya kupoteza uzima wa milele (1 Yoh. 2:3-6; 5:1-5; Zab. 119:155). Yesu aliye kielelezo chetu na ambaye ni Mungu alishika Amri Kumi za Baba yake; nasi kama wafuasi wake yatupasa kufuata kama yeye alivyoenenda(yohana15:10). Usikubali mtu ye yote akudanganye, maana "watu wabaya na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika" (2 Tim.3:13). Hao waepuke. Angalia usijidanganye mwenyewe (Gal. 6:7,8), wala usimruhusu kipofu akuongoze kipofu mwenzake, mtatumbukia wote wawili shimoni (Mt. 15:14). Uzima wa milele una thamani kubwa kiasi kwamba mtu hawezi kukubali kuupoteza vivi hivi (Mt. 22:29). Hapa tunawakuta vijana watatu wa Kiebrania kasoro Danieli hayupo safari hii. Katika Danieli 1 tuliona jinsi vijana wale wanne walivyoshinda mtihani ule wa chakula. Kula chakula au kunywa kinywaji kinachodhuru mwili kwa makusudi mazima ni kuvunja Amri ya Sita inayosema, Usiue(Kut.20:13).
Hivyo walishinda mtihani wa Amri ya Sita. Sasa wamekabiliwa na mtihani mgumu kabisa wa Amri ya Pili inayosema, "Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia. Usivisujudie wala kuvitumikia..." (Kutoka 20:4-6). Mfalme Nebukadreza baada ya kuelezwa maana ya ndoto yake aliyoota ya sanamu kubwa katika Danieli 2 kuhusu Falme zile Kuu Nne ukiwamo na ufalme wake akafanya shingo ngumu kupingana na Mungu.
Akatengeneza sanamu kubwa ya dhahabu tupu [dhahabu iliwakilisha ufalme wa Babeli] akimaanisha kwamba ufalme wa Babeli utadumu milele. Akataka sanamu hiyo iliyowekwa katika uwanda wa Dura isujudiwe na wote waliokuwapo pale (Dan.3:1-7).
Wote wakaisujudia kasoro wale vijana watatu Waebrania ----- Shadraka, Meshaki, na Abednego. Ni ujasiri ulioje katika halaiki ile walimokuwamo viongozi wakuu wa serikali ya Babeli! Watu wa Mungu wanatakiwa kuwa na ujasiri kama huo kutetea kweli ya Mungu hata kama mbingu zinadondoka
(Rum. 8:3539; Ebr. 11:32-40; Dan. 11:33).
Mfalme alijaribu kuwasihi wafanye hivyo mara watakaposikia tena filimbi na ngoma zikipigwa. Akawatishia kuwa atawatupa katika tanuru ya moto iliyokuwa kali mara saba kuliko kawaida. Lakini wao kwa upole wakasema, "Mfalme, Ee Nebukadreza, hamna haja kujibu katika neno hili. Kama ni hivyo, Mungu wetu tunayemtumikia aweza kutuokoa na tanuru ile iwakayo moto; naye atatuokoa na mkono wako, Ee mfalme. Bali kama si hivyo, ujue, Ee mfalme, ya kuwa sisi hatukubali kuitumikia miungu yako, wala kuisujudia hiyo sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha" (Dan. 3:16-18). Ndipo mfalme akakasirika sana na kuamuru wafungwe na kutupwa na wanajeshi mashujaa ndani ya tanuru ile ya moto. Wale waliowatupa walikufa kwa ukali wa moto ule. Hatimaye wakafanikiwa kuwatupa katikati ya ile tanuru iliyowaka moto. Je! kulitokea nini?Loo! mfalme akashangaa, hatukutupa watu watatu, mbona wako wanne, na mmoja anakuwa kama mwana wa miungu [Yesu alikuwa pale kuwaokoa]. Ameahidi kuwa atakuwa pamoja na watu wake mpaka mwisho wa dahari (Mt. 28:20). Hata wakipita motoni au katika maji mengi atakuwa pale tayari kuwaokoa (Isaya 43:1,2). Alitimiza ahadi yake kwao katika tukio lile la kutisha. Wakawa wanatembea ndani ya moto bila kuungua. Walipotolewa nje ya tanuru ile "wakawaona watu hao, ya kuwa ule moto ulikuwa hauna nguvu juu ya miili yao, wala nywele za vichwa vyao hazikuteketea, wala suruali zao hazikubadilika, wala harufu ya moto haikuwapata hata kidogo" (Dan. 3:27). Bwana asifiwe!!! Ana uweza wa kuokoa kabisa! Mungu anasema, "kwa maana wao wanaoniheshimu nitawaheshimu, na wao wanaonidharau watahesabiwa kuwa si kitu" (1 Sam. 2:30). Ndugu yangu, je! utasimama imara kutetea Amri Kumi za Mungu? Mfalme akatambua kuwa "hakuna Mungu mwingine awezaye kuokoa namna hii. Kisha akawakuza [akawapandisha cheo] Shadraka, na Meshaki, na Abednego, katika wilaya ya Babeli" (Dan. 3:29,30); akawadharau wale wote walioisujudu sanamu ile na kutoa amri kuwa wakisema neno lo lote juu ya Mungu wa vijana hao watakatwa vipande vipande na nyumba zao zitafanywa jaa [la takataka]. Hiyo si dharau kubwa? Kuna thawabu katika kusimama imara kutetea kweli ya Mungu. Yusufu alifungwa gerezani kwa kukataa kuzini, yaani, kuvunja Amri ya Saba (Kut. 20:14). Matokeo yake Mungu alikuwa naye gerezani na hatimaye alitolewa na kuheshimiwa kwa kupewa cheo cha Waziri Mkuu wa Misri (Mwa.39:21-23; 41:37-44). Babeli inawakilisha nguvu za giza [Shetani] zinazopigana na Amri Kumi za Mungu. Hata Babeli Mkuu wa Ufunuo anayo tabia iyo hiyo. Shetani anaitumia Babeli kutekeleza maangamizi yake juu ya watu wa Mungu wasio na hatia. Kizazi hiki cha mwisho cha Sayansi na Teknolojia kitakabiliwa na Mtihani Mgumu kuliko yote wa Amri ya Nne ihusuyo Sabato (Kut. 20:8-11). Yohana alionyeshwa kwamba kila mtu aliye hai wakati huo atajaribiwa (Ufu. 3:10). Watakaolindwa na Kristo ni wale waliolishika neno la subira yake (Ufu.14:12) ---- "Hapa ndipo penye subira ya watakatifu, hao wazishikao Amri [Kumi] za Mungu na Imani ya Yesu".
Je! utasimama chini ya Bendera ya Imanueli iliyoandikwa maneno hayo juu [Ufu. 14:12] au chini ya Bendera ya Chapa ya Mnyama [Ufu. 13:16,17] ----- iliyoandikwa siku ya kupumzika ya kizazi kipya kijacho?
Hebu kwa neema yake Mungu na tuazimie kwamba 'hatuwezi kutenda neno lo lote kinyume cha kweli, bali kwa ajili ya kweli" (2 Kor. 13:8). Lakini kweli ni nini? Neno la Mungu ni kweli; Sheria ya Mungu (Amri Kumi) ni kweli (Yoh. 17:17; Zab. 119:142).
Neno lake na Sheria yake hudumu milele (Mt. 25:35; 1 Pet. 1:23; Luka 16:17; Zab. 119:44).
Sheria yake ni "kamilifu"; hivyo huwezi kuongeza wala kupunguza kitu katika Sheria hiyo ya Amri Kumi (Zab. 19:7; Kum. 4:2,10-13).
Ndugu Mpendwa kama tulivyoona kwa kupitia somo ,muda sio mrefu ufalme wa rumi utasimama tena na kuamuru wanadamu wote kuisujudia alama ya mnyama manayeke ni kukubali kuabudu siku ya kwanza ya Juma (jumapili) .badala ya Juma mosi ,nikama vile wale vijana waebrania wakati wakiwa babeli walikuwa wamefundishwa kumtumikia Mungu na kumcha pekee bila kukengeushwa na mafundisho mengine kama yalivyo leo ,ndugu nnakuomba ukubali kujifunza neno la Mungu kwa kuzifahamu hasa vyema amri zake kumi (KUTOKA 20:3-17.)huwezi kuelewa kwa urahisi uhusiano uliopo kati ya amri kumi na wokovu ,Karibu kwa kanisa linalofundisha amri zote kumi kanisa la waadventista wa Sabato popote ulipo waweza kulipata kama utakuwa na swali juu ya masomo haya tahadhali usisite kuuliza .
Ninakukaribisha kwa somo linalofuata ambalo nimhimu sana kwa hatima ya maisha YETU .Bwana akubariki sana .
ConversionConversion EmoticonEmoticon