ZAMA ZA GIZA ZAANZA
Kule kujipatia mamlaka yake lile Kanisa la Roma ndio mwanzo wa Zama za Giza. Kadiri uwezo wake ulivyozidi kuongezeka, ndivyo giza [yaani, ujinga wa kutoijua Biblia, Sayansi na Teknolojia] lilivyozidi kuwa nene. Imani ikahamishwa kutoka kwa Kristo, aliye msingi wa kweli, kwenda kwa papa wa Roma. Badala ya kumtegemea Mwana wa Mungu kwa msamaha wa dhambi na wokovu ule wa milele, watu wakamtazama papa, na makasisi (mapadre) na maaskofu ambao alikuwa amewakabidhi mamlaka.
Wakafundishwa ya kwamba papa alikuwa ndiye mpatanishi wao wa kibinadamu na ya kwamba hakuna hata mmoja ambaye angeweza kumwendea Mungu isipokuwa kwa kupitia kwake, na kwa ajili hiyo yeye alipaswa kupewa utii bila swali lo lote. Kwenda kinyume na matakwa yake ilikuwa ni sababu ya kutosha ya kutolewa adhabu kali sana juu ya miili na roho za wale wahalifu. Kwa njia hiyo, mawazo ya watu yakageuziwa mbali na Mungu na kuelekezwa kwa wanadamu wawezao kukosa, kupotoka, na wakatili, naam, zaidi sana, kwa yule mkuu wa giza mwenyewe [Shetani], ambaye alitumia uwezo wake kupitia kwa watu wale. Dhambi ikafichwa katika vazi la utakatifu.
Maandiko yanapozuiwa kusomwa na watu, na mwanadamu anapokuja kujiona mwenyewe kuwa ni mkubwa kuliko wote, hapo ndipo tunapohitaji tu kutazamia kuona hila, udanganyifu, na uovu unaoishusha hadhi ya mwanadamu. Katika kuzitukuza sheria za wanadamu na mapokeo ukaonekana ufisadi ambao hutokea daima wakati Sheria ya Mungu [Amri Kumi] inapowekwa kandoSiku za Hatari Kubwa Kristo.
Zile zilikuwa ni siku za hatari kubwa kwa Kanisa lake Waaminifu walioibeba bendera yake walikuwa ni wachache kweli kweli.
Ingawa ile kweli haikuachwa bila kuwapo mashahidi, hata hivyo, wakati fulani ilionekana kana kwamba mafundisho yale ya uongo na ushirikina yalikuwa yameenea kote, na dini ile ya kweli ilionekana kana kwamba ingeweza kufutiliwa mbali duniani kote. Injili ikawa imesahauliwa, lakini mitindo ya dini ikaongezeka, na watu wakawa wamelemewa na mizigo mizito waliyotwishwa yenye masharti makali. Wakafundishwa sio tu kumtazama papa kama ndiye mpatanishi wao, bali kutegemea matendo yao wenyewe ili kuweza kulipa fidia ya dhambi zao. Safari ndefu za taabu kwenda kuzuru patakatifu, kutenda matendo ya kitubio, kuabudu mifupa ya watakatifu waliokufa zamani, kujenga makanisa, kujenga makaburi ya watakatifu, na altare [madhabahu], kulipa fedha nyingi kwa kanisa - mambo hayo pamoja na matendo mengine yanayofanana na hayo yaliamriwa ili kuituliza ghadhabu ya Mungu au kupata upendeleo wake, kana kwamba Mungu alikuwa kama wanadamu, kuweza kukasirishwa kwa mambo madogo sana yasiyo na maana, au kutulizwa kwa kupewa zawadi au kwa maungamo (kitubio)!
Giza lile likaonekana kana kwamba lilikuwa likiongezeka kuwa nene zaidi. Ibada ya sanamu ikawa ni jambola kawaida kwa watu wengi. Mishumaa ikawashwa mbele ya sanamu zile na sala zikatolewa kwa sanamu zile.
Desturi zile za kipuuzi kabisa na za kishirikina, hata akili zao zenyewe zikaonekana kana kwamba zimepoteza uwezo wake wa kujitawala. Wakati wale makasisi (mapadre) na maaskofu wenyewe walikuwa wanapenda anasa, uasherati, na ufisadi, iliweza kutazamiwa tu kwamba, watu wale waliowategemea kwa uongozi wao, nao wangeweza kuzama katika ujinga na uovu wao.
Papa yule Mwenye Majivuno Hatua nyingine katika dhana za kipapa ilichukuliwa katika karne ile ya kumi na moja wakati Papa Gregori wa Saba alipotangaza ukamilifu wa Kanisa la Roma.
Miongoni mwa mawazo yake aliyotoa lilikuwapo wazo moja lililosema kwamba kanisa lile [la Roma] lilikuwa halijapata kukosea kamwe kulingana na Maandiko. Lakini ushuhuda wa Maandiko hayo haukuambaatana na lile dai lake. Papa yule mwenye majivuno mengi alidai pia kwamba anao uwezo wa kuwaondoa wafalme katika kiti chao cha enzi, kisha akatangaza kwamba hakuna hukumu yo yote aliyoitoa yeye ambayo ingeweza kubatilishwa [kugeuzwa] na mtu ye yote, ila kwamba yeye ndiye alikuwa na haki ya kuyabatilisha [kuyageuza] maamuzi ya wengine wote. Ni tofauti kubwa ya kushangaza mno jinsi gani kati ya kiburi kile kilichojaa uonevu cha papa yule mwenye majivuno mengi ukilinganisha na upole na unyenyekevu wa moyo aliokuwa nao Kristo, ambaye anajiwakilisha mwenyewe kama mmoja anayebisha katika mlango wa moyo akiomba kuingia ndani, ili apate kuingia humo na kuleta msamaha na amani, na ambaye aliwafundisha wanafunzi wake, akasema: “Na mtu ye yote anayetaka kuwa wa kwanza kwenu na awe mtumwa wenu.” Mathayo 20:27
Giza Lazidi Kuwa Nene Karne zile zilipozidi kusonga mbele zilishuhudia ongezeko la daima la uongo katika mafundisho ya dini yaliyotolewa kutoka Roma.
Hata kabla ya kuanzishwa kwa upapa mafundisho ya wanafalsafa wale makafiri yalikuwa yamezingatiwa, nayo yalitoa mvuto wake ndani ya kanisa.
Wengi waliodai kwamba wameongoka walikuwa bado wanazing'ang'ania itikadi za falsafa yao ya kipagani, na si kwamba tu waliendelea kujifunza falsafa hiyo wao wenyewe, bali waliwashurutisha wengine kuipokea kama njia ya kueneza mvuto wao miongoni mwa makafiri wale.
Makosa mazito yakaingizwa kwa njia hiyo katika imani ya Kikristo. Lililojitokeza sana katika hayo ni ile imani kwamba mwanadamu ana roho isiyokufa, na ya kwamba, akifa bado anaendelea kuwa na fahamu zake. Fundisho hilo la dini likaweka msingi ambao juu yake Roma ilianzisha sala kwa ajili ya watakatifu waliokufa na ibada ya Bikira Maria. Kutokana na fundisho hilo pia ukazuka uzushi uliosema kwamba wale ambao hatimaye hawataweza kutubu wataendelea kuteswa motoni milele hata milele, fundisho ambalo liliingizwa katika imani ya kipapa.Ndipo njia ikawa imetayarishwa ya kuingizwa [kanisani] mavumbuzi mengine ya kipagani ambayo Roma iliyaita kwa jina la 'Toharani' (purgatory), nao wakalitumia fundisho hilo kuwatisha makundi ya watu wale waliokuwa wajinga na washirikina. Kwa uzushi wao huo, wanathibitisha kwamba pako mahali pa mateso, ambapo roho za wale wasiostahili adhabu ya milele zinapaswa kuadhibiwa kwa ajili ya dhambi zao, na ya kwamba, kutoka hapo, zinapowekwa huru mbali na uchafu wake, roho hizo huingizwa mbinguni.
Aksante kwa kufuatilia haya masomo hakika ndivyo ulivyo ukweli amua kuufahamu zaidi utakuweka huru kisha Fanya maamuzi ya kuufuata Mungu akubariki karibu kwa somo linalifuata.
Kule kujipatia mamlaka yake lile Kanisa la Roma ndio mwanzo wa Zama za Giza. Kadiri uwezo wake ulivyozidi kuongezeka, ndivyo giza [yaani, ujinga wa kutoijua Biblia, Sayansi na Teknolojia] lilivyozidi kuwa nene. Imani ikahamishwa kutoka kwa Kristo, aliye msingi wa kweli, kwenda kwa papa wa Roma. Badala ya kumtegemea Mwana wa Mungu kwa msamaha wa dhambi na wokovu ule wa milele, watu wakamtazama papa, na makasisi (mapadre) na maaskofu ambao alikuwa amewakabidhi mamlaka.
Wakafundishwa ya kwamba papa alikuwa ndiye mpatanishi wao wa kibinadamu na ya kwamba hakuna hata mmoja ambaye angeweza kumwendea Mungu isipokuwa kwa kupitia kwake, na kwa ajili hiyo yeye alipaswa kupewa utii bila swali lo lote. Kwenda kinyume na matakwa yake ilikuwa ni sababu ya kutosha ya kutolewa adhabu kali sana juu ya miili na roho za wale wahalifu. Kwa njia hiyo, mawazo ya watu yakageuziwa mbali na Mungu na kuelekezwa kwa wanadamu wawezao kukosa, kupotoka, na wakatili, naam, zaidi sana, kwa yule mkuu wa giza mwenyewe [Shetani], ambaye alitumia uwezo wake kupitia kwa watu wale. Dhambi ikafichwa katika vazi la utakatifu.
Maandiko yanapozuiwa kusomwa na watu, na mwanadamu anapokuja kujiona mwenyewe kuwa ni mkubwa kuliko wote, hapo ndipo tunapohitaji tu kutazamia kuona hila, udanganyifu, na uovu unaoishusha hadhi ya mwanadamu. Katika kuzitukuza sheria za wanadamu na mapokeo ukaonekana ufisadi ambao hutokea daima wakati Sheria ya Mungu [Amri Kumi] inapowekwa kandoSiku za Hatari Kubwa Kristo.
Zile zilikuwa ni siku za hatari kubwa kwa Kanisa lake Waaminifu walioibeba bendera yake walikuwa ni wachache kweli kweli.
Ingawa ile kweli haikuachwa bila kuwapo mashahidi, hata hivyo, wakati fulani ilionekana kana kwamba mafundisho yale ya uongo na ushirikina yalikuwa yameenea kote, na dini ile ya kweli ilionekana kana kwamba ingeweza kufutiliwa mbali duniani kote. Injili ikawa imesahauliwa, lakini mitindo ya dini ikaongezeka, na watu wakawa wamelemewa na mizigo mizito waliyotwishwa yenye masharti makali. Wakafundishwa sio tu kumtazama papa kama ndiye mpatanishi wao, bali kutegemea matendo yao wenyewe ili kuweza kulipa fidia ya dhambi zao. Safari ndefu za taabu kwenda kuzuru patakatifu, kutenda matendo ya kitubio, kuabudu mifupa ya watakatifu waliokufa zamani, kujenga makanisa, kujenga makaburi ya watakatifu, na altare [madhabahu], kulipa fedha nyingi kwa kanisa - mambo hayo pamoja na matendo mengine yanayofanana na hayo yaliamriwa ili kuituliza ghadhabu ya Mungu au kupata upendeleo wake, kana kwamba Mungu alikuwa kama wanadamu, kuweza kukasirishwa kwa mambo madogo sana yasiyo na maana, au kutulizwa kwa kupewa zawadi au kwa maungamo (kitubio)!
Giza lile likaonekana kana kwamba lilikuwa likiongezeka kuwa nene zaidi. Ibada ya sanamu ikawa ni jambola kawaida kwa watu wengi. Mishumaa ikawashwa mbele ya sanamu zile na sala zikatolewa kwa sanamu zile.
Desturi zile za kipuuzi kabisa na za kishirikina, hata akili zao zenyewe zikaonekana kana kwamba zimepoteza uwezo wake wa kujitawala. Wakati wale makasisi (mapadre) na maaskofu wenyewe walikuwa wanapenda anasa, uasherati, na ufisadi, iliweza kutazamiwa tu kwamba, watu wale waliowategemea kwa uongozi wao, nao wangeweza kuzama katika ujinga na uovu wao.
Papa yule Mwenye Majivuno Hatua nyingine katika dhana za kipapa ilichukuliwa katika karne ile ya kumi na moja wakati Papa Gregori wa Saba alipotangaza ukamilifu wa Kanisa la Roma.
Miongoni mwa mawazo yake aliyotoa lilikuwapo wazo moja lililosema kwamba kanisa lile [la Roma] lilikuwa halijapata kukosea kamwe kulingana na Maandiko. Lakini ushuhuda wa Maandiko hayo haukuambaatana na lile dai lake. Papa yule mwenye majivuno mengi alidai pia kwamba anao uwezo wa kuwaondoa wafalme katika kiti chao cha enzi, kisha akatangaza kwamba hakuna hukumu yo yote aliyoitoa yeye ambayo ingeweza kubatilishwa [kugeuzwa] na mtu ye yote, ila kwamba yeye ndiye alikuwa na haki ya kuyabatilisha [kuyageuza] maamuzi ya wengine wote. Ni tofauti kubwa ya kushangaza mno jinsi gani kati ya kiburi kile kilichojaa uonevu cha papa yule mwenye majivuno mengi ukilinganisha na upole na unyenyekevu wa moyo aliokuwa nao Kristo, ambaye anajiwakilisha mwenyewe kama mmoja anayebisha katika mlango wa moyo akiomba kuingia ndani, ili apate kuingia humo na kuleta msamaha na amani, na ambaye aliwafundisha wanafunzi wake, akasema: “Na mtu ye yote anayetaka kuwa wa kwanza kwenu na awe mtumwa wenu.” Mathayo 20:27
Giza Lazidi Kuwa Nene Karne zile zilipozidi kusonga mbele zilishuhudia ongezeko la daima la uongo katika mafundisho ya dini yaliyotolewa kutoka Roma.
Hata kabla ya kuanzishwa kwa upapa mafundisho ya wanafalsafa wale makafiri yalikuwa yamezingatiwa, nayo yalitoa mvuto wake ndani ya kanisa.
Wengi waliodai kwamba wameongoka walikuwa bado wanazing'ang'ania itikadi za falsafa yao ya kipagani, na si kwamba tu waliendelea kujifunza falsafa hiyo wao wenyewe, bali waliwashurutisha wengine kuipokea kama njia ya kueneza mvuto wao miongoni mwa makafiri wale.
Makosa mazito yakaingizwa kwa njia hiyo katika imani ya Kikristo. Lililojitokeza sana katika hayo ni ile imani kwamba mwanadamu ana roho isiyokufa, na ya kwamba, akifa bado anaendelea kuwa na fahamu zake. Fundisho hilo la dini likaweka msingi ambao juu yake Roma ilianzisha sala kwa ajili ya watakatifu waliokufa na ibada ya Bikira Maria. Kutokana na fundisho hilo pia ukazuka uzushi uliosema kwamba wale ambao hatimaye hawataweza kutubu wataendelea kuteswa motoni milele hata milele, fundisho ambalo liliingizwa katika imani ya kipapa.Ndipo njia ikawa imetayarishwa ya kuingizwa [kanisani] mavumbuzi mengine ya kipagani ambayo Roma iliyaita kwa jina la 'Toharani' (purgatory), nao wakalitumia fundisho hilo kuwatisha makundi ya watu wale waliokuwa wajinga na washirikina. Kwa uzushi wao huo, wanathibitisha kwamba pako mahali pa mateso, ambapo roho za wale wasiostahili adhabu ya milele zinapaswa kuadhibiwa kwa ajili ya dhambi zao, na ya kwamba, kutoka hapo, zinapowekwa huru mbali na uchafu wake, roho hizo huingizwa mbinguni.
Aksante kwa kufuatilia haya masomo hakika ndivyo ulivyo ukweli amua kuufahamu zaidi utakuweka huru kisha Fanya maamuzi ya kuufuata Mungu akubariki karibu kwa somo linalifuata.
ConversionConversion EmoticonEmoticon