ONYO LA MWISHO WA DUNIA SEHEMU YA TATU.

Je, Roma Itatawala Ulimwengu Tena?

Hili ni swali ambalo kila mmoja wetu leo bila ushabiki wala ubishi imetupasa kurejea katika unabii ili tujue zaidi nini hasa ukweli ulivyo, hebu tuiangalie kidogo historia kwa ufupi hapa. KANISA LA MTAKATIFU PETRO, ROMA

Maridhiano ya Kufisha,
 Mtume  Paulo,  katika  Waraka  wake  wa  Pili  kwa Wathesalonike,  alitabiri  juu  ya  uasi  mkuu  ambao  ungeleta matokeo  ya  kuianzisha  mamlaka  ile  ya  upapa.   Alitangaza kwamba  siku  ile  ya  kuja  Kristo  isingeweza  kuja,  “usipokuja kwanza  ule  ukengeufu;  akafunuliwa  mtu  yule  wa  dhambi (kuasi),  mwana  wa  uharibifu;   yule  Mpingamizi  [Mpinga Kristo],  ajiinuaye  nafsi  yake  juu  ya  kila  kiitwacho  Mungu  ama kuabudiwa;   hata  yeye  mwenyewe  kuketi  katika  hekalu  [kanisa] la  Mungu,  akijionyesha  nafsi  yake  kana  kwamba  yeye  ndiye Mungu.”    Tena,  zaidi  ya  hayo,  Mtume  huyo  anawaonya  ndugu zake  kwamba  “ile  siri  ya  kuasi  hivi  sasa  inatenda  kazi.”   2 Wakorintho  2:3,4,7.  

Hata  katika  kipindi  kile  cha  mwanzo kabisa  aliona  yakiingia  ndani  ya  kanisa  mafundisho  potofu ambayo yangetayarisha njia ya kujitokeza kwa upapa. Kidogo  kidogo,  mwanzoni  kwa  siri  na  kimya  kimya,  na baadaye  kwa  wazi  zaidi,  ikaongezeka  nguvu  yake  na  kuitawala mioyo  ya  wanadamu,  ile  “siri  ya  kuasi”  ikaiendeleza  mbele  kazi yake  kwa  kutumia  madanganyo  na  makufuru.   Karibu  bila kutambulikana  kabisa  desturi  zile  za  kikafiri  zikaingia  ndani  ya kanisa  la  Kikristo.  
 Roho  ile  ya  maridhiano  na  kufanana-fanana [na  dunia]  ilizuiwa  kwa  wakati  fulani  kutokana  na  mateso makali  ambayo  kanisa  lilistahimili  chini  ya  wapagani.  

Lakini mateso  yale  yalipokoma,  na  Ukristo  ulipoingia  katika  mabaraza na  majumba  ya  kifalme,  ndipo  kanisa  lile  lilipouweka  kando unyenyekevu  ule  wa  Kristo  na  Mitume  wake  na  kujitwalia ufahari  na  kiburi  cha  makuhani  na  watawala  wale  wa  kipagani; na  mahali  pa  matakwa  ya  Mungu  likaweka  nadharia  za wanadamu  pamoja  na  desturi  zao.  

Kuongoka  kwa  jina  tu  kwa Konstantino,  mapema  katika  karne  ile  ya  nne,  kulileta  shangwe kubwa;   na  ulimwengu  [upagani],  ukiwa  umevikwa  joho  la mfano  wa  haki,  ukatembea  na  kuingia  ndani  ya  kanisa.  
 Basi, kazi  ile  ya  uharibifu  ikasonga  mbele  kwa  haraka  sana.   Upagani, wakati  ukionekana  kana  kwamba  umeshindwa  kabisa,  ukawa ndio  mshindi.  
Roho  yake  ikalitawala  kanisa  lile.   Mafundisho yake  ya  dini,  sherehe  zake,  na  ushirikina  wake  vikaingizwa katika  imani  na  ibada  ya  wale  waliojidai  kuwa  ni  wafuasi  wake Kristo.
Mtu wa Dhambi Maridhiano  hayo  kati  ya  Upagani  na  Ukristo  yalikuwa  na matokeo  ya  kujitokeza  kwa  “mtu  yule  wa  dhambi”  (man  of  sin) ambaye  alitabiriwa  katika  unabii  huo  kuwa  atakuwa  Mpingamizi [Mpinga  Kristo],  na  ya  kwamba  atajiinua  mwenyewe  juu  ya Mungu.   Mfumo  huo  mkubwa  kabisa  wa  dini  ya  uongo  ni  kazi kuu  ya  kilele  ya  uwezo  wake  Shetani   -   yaani,  ni  kielelezo  bora kabisa  cha  kazi  ile  inayostahili  kukumbukwa  ambayo  inatokana na  juhudi  zake  [Shetani]  za  kujiketisha  yeye  mwenyewe  juu  ya kiti cha enzi ili kuitawala dunia hii kama apendavyo yeye.
Siku  moja  Shetani  alijitahidi  sana  kufanya  maridhiano  na Kristo.   Akaja  kwa  Mwana  wa  Mungu  katika  nyika  ile  ya majaribu,  na  kumwonyesha  falme  zote  za  dunia  hii  pamoja  na utukufu  wake,  na  kujitolea  kumpa  vyote  mikononi  mwake  mradi tu  akubali  kwamba  mkuu  yule  wa  giza  [Shetani]  ndiye  mwenye mamlaka  yote.   Kristo  alimkemea  mjaribu  yule  mwenye  kiburi na  kumlazimisha  kuondoka  pale.  
Lakini  Shetani  anapata mafanikio  makubwa  sana  anapoyaleta  majaribu  yale  yale  kwa mwanadamu.   Ili  kujipatia  manufaa  na  heshima  za  ulimwengu huu,  kanisa  lile  likatafuta  upendeleo  na  kuungwa  mkono  na wakuu  wa  dunia  hii;   na  kwa  njia  hiyo,  likiwa  limemkana  Kristo, likashawishiwa  kutoa  utii  wake  kwa  mwakilishi  yule  wa  Shetani-  yaani, kwa Askofu [Papa] yule wa Roma.
Msingi wa Fundisho Hilo la Uongo Ni  mojawapo  la  mafundisho  makuu  ya  dini  ile  ya Kiroma  kwamba  papa  ni  kichwa  kinachoonekana  kwa  macho cha  kanisa  la  ulimwengu  mzima  la  Kristo,  kwamba  amepewa mamlaka  ya  juu  kabisa  juu  ya  maaskofu  na  wachungaji  wote katika  sehemu  zote  za  dunia  hii.   Zaidi  ya  hayo,  papa  amepewa vyeo  vya  Mungu.   Amepewa  cheo  cha  “Bwana  Mungu  Papa,” tena  ametangazwa  kuwa  hawezi  kukosea  kamwe.   Anadai kwamba  wanadamu  wote  wanapaswa  kumsujudu  yeye.   Dai  lile lile  alilolisisitiza  Shetani  katika  nyika  ile  ya  majaribu  bado linasisitizwa  naye  [papa]  kupitia  katika  Kanisa  la  Roma,  na  idadi kubwa sana ya watu wako tayari kumsujudu yeye. “Tunashikilia hapa duniani mahali pa Mungu Mwenyezi." Papa Leo wa 13, Katika  Barua  yake  ya  Utume, Juni  20,  1894. Lakini  wale  wanaomcha  na  kumheshimu  Mungu,  kama vile  Kristo  alivyopambana  na  ubembelezi  wa  yule  adui mwerevu,  wanapambana  na  madai  hayo  yatokanayo  na ushupavu  wake  wa  kujinyakulia  vyeo  vya  Mungu,  wakisema: “Msujudie  Bwana  Mungu  wako,  umwabudu  yeye  peke  yake.” Luka  4:8.   Mungu  hajatoa  dokezo  lo  lote  katika  Neno  lakelisemalo  kwamba  amemchagua  mwanadamu  fulani  kuwa kichwa  cha  kanisa  lake.  
Fundisho  la  dini  la  ukuu  wa  papa  usio na  kifani  hupingana  moja  kwa  moja  na  mafundisho  ya Maandiko.   Papa  hawezi  kuwa  na  mamlaka  yo  yote  juu  ya Kanisa la Kristo isipokuwa kwa utapeli. Wafuasi  wa  papa  wamekazana  sana  kuleta  mashtaka  ya uzushi  dhidi  ya  Waprotestanti  na  dhidi  ya  kujitenga  kwao  kwa makusudi  toka  katika  kanisa  lao  la  kweli.   Lakini  mashtaka  hayo ndiyo  hasa  yanayowahusu  wao  wenyewe.   Wao  ndio  walioitupa chini  bendera  ya  Kristo  na  kujitenga  mbali  na  ile  “imani waliyokabidhiwa watakatifu mara moja tu.”  Yuda 3.Mgunduzi wa Mafundisho ya Uongo Shetani  alijua  fika  ya  kwamba  Maandiko  yale  Matakatifu yangewawezesha  wanadamu  kuyang’amua  madanganyo  yake  na kuupinga  uwezo  wake.   Ilikuwa  ni  kwa  njia  ya  Neno  hilo  hata yule  Mwokozi  wa  ulimwengu  aliweza  kuyapinga  mashambulio yake.   Kwa  kila  shambulio  lake  [Shetani],  Kristo  alionyesha ngao  ya  ile  kweli  ya  milele,  akisema,  “Imeandikwa.”   Kwa  kila shauri  alilotoa  yule  adui,  alikataa  kwa  kutegemea  hekima  na uwezo  wa  lile  neno.   Ili  huyo  Shetani  apate  kudumisha  utawala wake  juu  ya  wanadamu,  na  kuimarisha  mamlaka  ya  tapeli  yule wa  kipapa,  ilikuwa  ni  lazima  kwake  kuwaweka  watu  katika  hali ya  ujinga  wa  kutoyajua  Maandiko.   Biblia  ingemtukuza  Mungu na  kuwaweka  wanadamu  mahali  pao  panapowastahili  hasa;   kwa hiyo  ilikuwa  ni  lazima  kwamba  zile  kweli  zake  takatifu  zifichwe kwa  watu  na  kupigwa  marufuku.   Mantiki  hiyo  ikatumiwa  na Kanisa  la  Roma.   Kwa  mamia  ya  miaka  uenezaji  wa  Biblia ulipigwa  marufuku.   Watu  walikatazwa  kuisoma  au  kuwa  nayo katika  nyumba  zao,  na  makasisi  (mapadre)  pamoja  na  maaskofu wapotovu  wakayafafanua  mafundisho  yake  ili  yapate  kuunga mkono  unafiki  wao.  Hivyo  ndivyo  papa  alivyokuja kutambulikana  karibu  ulimwenguni  kote  kama  Kaimu  wa  [Aliye Badala  ya]  Mungu  hapa  duniani,  ambaye  alipewa  mamlaka  juu ya kanisa na serikaliKuelewa Unakokwenda Upapa, Angalia Historia Yake IliyopitaKuupigia Magoti Upagani Baada  ya  kuondolewa  yule  anayegundua  mafundisho potofu  [yaani,  Biblia],  Shetani  akafanya  kama  apendavyo. Unabii  ulikuwa  umetangaza  kwamba  upapa  unge“azimu kubadili  majira  na  Sheria  [Amri  Kumi].”   Danieli  7:25.   Kazi hiyo  [upapa]  haukuchelewa  kuanza  kuifanya.   Ili  kuwapa waongofu  waliotoka  kwenye  upagani  kitu  fulani  badala  ya  ibada yao  ya  sanamu,  na  kukuzia  upokeaji  wao  wa  Ukristo  kwa  jina  tu, kuabudu  sanamu  na  mabaki  ya  mifupa  ya  watakatifu  waliokufa zamani  vikaingizwa  taratibu  katika  ibada  ya  Kikristo.   Amri iliyotolewa  na  baraza  kuu  hatimaye  ikauimarisha  mfumo  huo  wa ibada  ya  sanamu.   Kuikamilisha  kazi  hiyo  ya  kukufuru,  Roma ikadhamiria  kuifutilia  mbali  kutoka  katika  Sheria  ya  Mungu [Amri  Kumi]  amri  ile  ya  pili  inayokataza  ibada  ya  sanamu,  na kuigawa  amri  ile  ya  kumi  ili  kuhifadhi  idadi  ile  ile  [ya  Amri Kumi].
Previous
Next Post »