Mpendwa ninakukaribisha tena katika siku ya leo katika mfululizo wa masomo kutoka katika kitabu cha Daniel ,leo tutaangalia jinsi kiburi juu ya neno la Mungu kinavyoleta athali na Hatari , ukizingatia masomo ya hapo awali tuliona kwamba shetani ndiye baba wa uongo ,ndiye anayejenga kiburi juu ya uzima wa milele , Bwana ashukuriwe maana anaweza kubadiri kila kitu. Hebu soma hii sura ilitwende kwa pamoja kwa hili somo
(SOMA DANIELI 4 YOTE)
Hivi unadhani kiburi hutokana na nini ,kwa ufupi kinatokana na nafsi, yaani, umimi. Kiini cha dhambi zote ni ule umimi (nafsi). Unaweza kujikweza au unaweza kujidhalilisha isivyopasa. Mambo yote hayo mawili ni kiburi. Mwenye kujikweza anasema, "Mimi ni tajiri, mimi ni msomi, mimi... mimi...." Anajiona kuwa yu bora kuliko wengine kwa vile alivyo na kwa vile anavyofanya. Anayejidhalilisha isivyopasa akipongezwa kwa kazi nzuri aliyofanya, anasema, "Si kitu! Sikufanya la maana!...." Lakini moyoni mwake anajipongeza kuwa amefanya vizuri sana. Yule anayesoma mioyo anaandika katika kumbukumbu kuwa hicho ni kiburi. Kiburi kilimwangusha Lusifa mbinguni akapewa jina baya la Shetani
(Isa. 14:12-15; Eze. 28:14-17). Wazazi wetu Bustanini Edeni walidanganywa na Shetani kuwa wakila tunda lile lililokatazwa watakuwa kama Mungu. Wakala, wakajiona uchi, wakapoteza utukufu walioumbiwa nao, na wazao wao wakawa wamepungukiwa na utukufu huo (Mwa. 3:3-7; Rum.3:23). Mungu anachukia sana kiburi kwa sababu nafsi yetu inataka kumwondoa katika kiti chake cha enzi mioyoni mwetu na kukikalia yenyewe (Mithali 6:1619). Tulijifunza katika somo la kwanza (Danieli 1) kwamba miili yetu ni Hekalu la Roho Mtakatifu. Mtu anayeiruhusu nafsi kutawala moyo wake anamfukuza Roho moyoni mwake. Kama kuna vita kali kuliko zote hapa duniani ni ile ya kupigana na nafsi yetu.
Nafsi haifi kabisa; inaweza kukandamizwa tu isijitutumue. Kwa hiyo ni muhimu kuwa macho kila wakati ili isije ikajitutumua juu ya Mungu au juu ya watu wengine. Paulo alikuwa na vita iyo hiyo. Anasema, "Ninakufa kila siku"
(1Kor. 15:31).
Kwa maneno mengine, "naifisha nafsi yangu kila siku," au "napigana na umimi unaojiinua ndani yangu." Kuweza kuidhibiti nafsi ni kwa njia ya kumruhusu Kristo kukaa moyoni mwetu, "Nimesulibiwa pamoja na Kristo; lakini ni hai; wala si mimi [si umimi wangu] tena, bali Kristo yu hai ndani yangu; na uhai nilio nao sasa katika mwili, ninao katika imani ya Mwana wa Mungu, ambaye alinipenda akajitoa nafsi yake kwa ajili yangu" (Gal. 2:20).
Nafsi itaondolewa ndani yetu wakati wa parapanda ya mwisho tutakapopewa miili ya utukufu, isiyokufa (1 Kor. 15:51-53).
Ndiyo maana si vizuri mtu kujisifu kuwa ameokoka, maana anaweza kuangushwa na nafsi wakati wo wote na kupoteza wokovu wake (1 Kor. 10:12; Eze. 33:12-16; Mt. 24:13).
Kwanza kule kujisifu kwenyewe tu ni dhambi ambayo haina msamaha mpaka mtu huyo atubu na kujishusha kiburi chake (Luka 18:9-14).
Tunaruhusiwa kujisifia msalaba wa Kristo tu uliotuletea ukombozi sisi tusiostahili (Gal.6:14). Sifa zote anastahili kupewa Mungu kwa lo lote tufanyalo au kwa mafanikio yetu (Yer.9:23,24). Sasa tunamkuta mfalme Nebukadreza aliyekuwa ameuona uweza mkuu wa Mungu wa kuwaokoa wale vijana watatu katika tanuru ile ya moto, na kukiri kwamba "hakuna Mungu mwingine awezaye kuokoa namna hii" (Dan. 3:29), akijitukuza juu ya Mungu huyo kwa njia ya kiburi chake.
Mji wa Babeli ulikuwa na utukufu mkubwa sana (Isa. 13:19a).
Hakuna ufalme mwingine duniani unaoweza kuwa na utukufu kama ule. Mungu alimpa ndoto ya sanamu iliyowakilisha falme zote zitakazotawala kuanzia wakati wake mpaka Kristo atakapousimamisha ufalme wake (Danieli 2). Kwa kiburi akapinga mpango wa Mungu kwa kusimamisha sanamu ya dhahabu tupu (dhahabu iliwakilisha ufalme wa Babeli) katika uwanda wa Dura na kutaka watu waisujudie kama tulivyoona kwa somo la hapo nyuma . Kwa kiburi alimdharau Mungu wa mbinguni kuwa si kitu; bali kwamba yeye atadumu milele pamoja na ufalme wake. Aliishi na watu wa Mungu ili ajifunze juu ya Mungu wa Israeli; vijana wale wanne walikuwa fundisho kuu kwake. Hakujali yote hayo. Mungu katika upendo wake akamletea ndoto ya pili ili kumwonya aachane na kiburi chake sugu (Dan. 4:4-17).
Katika ndoto yake aliona mti mrefu uliokua mpaka mbinguni; wanadamu, wanyama, ndege wote walipata chakula chao katika mti huo. Kisha akamwona mlinzi mtakatifu akiamuru mti ule ukatwe kibaki kisiki tu kikapate umande wa mbinguni kwa nyakati (miaka) saba.
Kwa nini? "Kusudi walio hai wapate kujua ya kuwa Aliye juu anatawala katika ufalme wa wanadamu, naye humpa amtakaye, tena humtawaza juu yake aliye mnyonge" (Dan. 4:17). Ni wafalme wangapi wanaofahamu kuwa ni Mungu aliyewaweka katika viti vya enzi wanavyovikalia? hata leo tunapoona vitisho vya Vita baina ya mataifa ni kwa sababu wanasahau kwamba ni MUNGU aliyeruhusu wawe viongozi .
(Rum.13:1-7; 1 Tim. 2:1-6). Wajibu wa Serikali zote za dunia ni kusimamia utekelezaji wa Amri Sita za mwisho katika zile Kumi (Kut. 20:12-17).
Wanapofanya kazi yao hiyo vizuri na kwa uaminifu na haki mataifa yao yanabarikiwa. Wanapoingilia mambo yanayomhusu Mungu (Amri Nne za kwanza - Kut. 20:3-11) wanavuka mipaka ya madaraka aliyowapa na kustahili adhabu kutoka kwa Mungu.
Kumbuka kuwa Biblia sio kitabu cha siasa; lakini kuinuka na kuanguka kwa mataifa yote ya dunia kumeelezwa humo.
Ni Mungu anayetawala katika falme zote za wanadamu. Mungu anapima nyendo za mataifa yote duniani (Zab. 66:7-8; Zaburi 2; 9:17). Ni jambo la kusikitisha mno kwamba mataifa yote ya dunia, ukiwaondoa watakatifu waliomo, yataangamizwa vibaya siku ile ya mwisho kwa kwenda kinyume na madaraka aliyowapa Mungu.
je ,wewe hapo ulipo unatenda haki kama kiongozi ?.
(Ufu. 19:11-21). Danieli alipoitwa kuitafsiri ndoto ile ya mfalme "akashangaa kwa muda, na fikara zake zikamfadhaisha" (Dan. 4:19). Kwa nini alifadhaika?
Kwa sababu ndoto ile ilimaanisha kwamba mfalme angefukuzwa mbali na wanadamu na kula majani kama ng'ombe kwa miaka saba. Kwa nini iwe hivyo? Kwa sababu ya kiburi chake sugu. "Nyakati [miaka] saba zitapita juu yako; hata utakapojua ya kuwa Aliye juu ndiye anayemiliki katika ufalme wa wanadamu, naye humpa yeye amtakaye, awaye yote" (Dan. 4:25). Miezi 12 baadaye, "alikuwa akitembea ndani ya jumba la kifalme katika Babeli. Mfalme akanena, akasema, Mji huu sio Babeli mkubwa nilioujenga mimi, uwe kao langu la kifalme, kwa uwezo wa nguvu zangu, ili uwe utukufu wa enzi yangu?" (Dan. 4:29,30).
Unaona alivyokuwa anajisifu ? Pale pale tangazo likatolewa kutoka mbinguni kuwa ufalme wake umeondoka kwake na atakaa na wanyama akila majani kama ng'ombe kwa miaka saba mpaka atakapojifunza kumtambua Mungu wa mbinguni. Mafunzo ya miaka saba kukishusha kiburi sugu! Fikiria hilo! Mungu na ashukuriwe! Nebukadreza alijifunza kwa njia ya aibu sana (ya kuwa mwehu) kwa miaka saba mizima. Alitoka akiwa kiumbe kipya; akakitubia kiburi chake sugu na kuanzia hapo akaanza kumtukuza hadharani Mungu wa mbinguni (Dan. 4:34,35).
Ufalme wake akarudishiwa. Ushuhuda wake mbele za watu
ameutoa mwanzo wa Sura hii ya 4. "Mfalme Nebukadreza, kwa watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wanaokaa katika dunia yote; Amani iongezeke kwenu. Mimi nimeona vema kutangaza habari za ishara na maajabu, aliyonitendea Mungu aliye juu. Ishara zake ni kubwa kama nini! na maajabu yake yana uweza kama nini! ufalme wake ni ufalme wa milele; na mamlaka yake ni ya kizazi hata kizazi" (Dan. 4:1-3). Siku moja wale watakaookolewa watakutana na Nebukadreza mbinguni. Atawasimulia vizuri kisa chake.
Ni wangapi ambao Mungu anapozungumza nao katika Neno lake wanakaza shingo zao kwa kiburi na kuyatukuza mawazo yao juu ya Mungu na kufanya kinyume na maagizo yake? Je, wako tayari kupelekwa porini na kula majani ili wajifunze? Hilo ni zoezi kali mno. Je! Mungu atanivumilia mpaka lini asiukate mti wangu? (Luka 13:6-9). Yatupasa kutubu; la sivyo tutaangamizwa (Luka 13:1-5). Je, umewahi kufikilia juu ya kile ulichonacho unadhani ni nani aliyeruhisu ukipate ,je unamkumbuka Mungu kwa kukupatia usiseme ni kwaakiri zako maana pasipo yeye hatuwezi neno lolote.
Sisi si maarufu kuliko Mungu; wala sisi si bora kuliko wengine.hatuna haja ya kuwa wabishi pasipo sababu ,kuwa wenye viburi ,wasiotaka kubadirika mm Fredrick sylvanus ninaungana na wewe rafiki Mpendwa tushushe kiburi cha uzima tusisubiri kupata mapigo ndipo tujishushe ,leo nnakuarika Mpendwa ujitoe kwa YESU ndiye anayefundisha tabia njema ,ndiye anayetoa kiburi ,anarudisha na kuumba upya tabia njema ,Karibu umpokee YESU atakuweka huru Bwana akubariki ,
Karibu kwa somo linalofuata.
(SOMA DANIELI 4 YOTE)
Hivi unadhani kiburi hutokana na nini ,kwa ufupi kinatokana na nafsi, yaani, umimi. Kiini cha dhambi zote ni ule umimi (nafsi). Unaweza kujikweza au unaweza kujidhalilisha isivyopasa. Mambo yote hayo mawili ni kiburi. Mwenye kujikweza anasema, "Mimi ni tajiri, mimi ni msomi, mimi... mimi...." Anajiona kuwa yu bora kuliko wengine kwa vile alivyo na kwa vile anavyofanya. Anayejidhalilisha isivyopasa akipongezwa kwa kazi nzuri aliyofanya, anasema, "Si kitu! Sikufanya la maana!...." Lakini moyoni mwake anajipongeza kuwa amefanya vizuri sana. Yule anayesoma mioyo anaandika katika kumbukumbu kuwa hicho ni kiburi. Kiburi kilimwangusha Lusifa mbinguni akapewa jina baya la Shetani
(Isa. 14:12-15; Eze. 28:14-17). Wazazi wetu Bustanini Edeni walidanganywa na Shetani kuwa wakila tunda lile lililokatazwa watakuwa kama Mungu. Wakala, wakajiona uchi, wakapoteza utukufu walioumbiwa nao, na wazao wao wakawa wamepungukiwa na utukufu huo (Mwa. 3:3-7; Rum.3:23). Mungu anachukia sana kiburi kwa sababu nafsi yetu inataka kumwondoa katika kiti chake cha enzi mioyoni mwetu na kukikalia yenyewe (Mithali 6:1619). Tulijifunza katika somo la kwanza (Danieli 1) kwamba miili yetu ni Hekalu la Roho Mtakatifu. Mtu anayeiruhusu nafsi kutawala moyo wake anamfukuza Roho moyoni mwake. Kama kuna vita kali kuliko zote hapa duniani ni ile ya kupigana na nafsi yetu.
Nafsi haifi kabisa; inaweza kukandamizwa tu isijitutumue. Kwa hiyo ni muhimu kuwa macho kila wakati ili isije ikajitutumua juu ya Mungu au juu ya watu wengine. Paulo alikuwa na vita iyo hiyo. Anasema, "Ninakufa kila siku"
(1Kor. 15:31).
Kwa maneno mengine, "naifisha nafsi yangu kila siku," au "napigana na umimi unaojiinua ndani yangu." Kuweza kuidhibiti nafsi ni kwa njia ya kumruhusu Kristo kukaa moyoni mwetu, "Nimesulibiwa pamoja na Kristo; lakini ni hai; wala si mimi [si umimi wangu] tena, bali Kristo yu hai ndani yangu; na uhai nilio nao sasa katika mwili, ninao katika imani ya Mwana wa Mungu, ambaye alinipenda akajitoa nafsi yake kwa ajili yangu" (Gal. 2:20).
Nafsi itaondolewa ndani yetu wakati wa parapanda ya mwisho tutakapopewa miili ya utukufu, isiyokufa (1 Kor. 15:51-53).
Ndiyo maana si vizuri mtu kujisifu kuwa ameokoka, maana anaweza kuangushwa na nafsi wakati wo wote na kupoteza wokovu wake (1 Kor. 10:12; Eze. 33:12-16; Mt. 24:13).
Kwanza kule kujisifu kwenyewe tu ni dhambi ambayo haina msamaha mpaka mtu huyo atubu na kujishusha kiburi chake (Luka 18:9-14).
Tunaruhusiwa kujisifia msalaba wa Kristo tu uliotuletea ukombozi sisi tusiostahili (Gal.6:14). Sifa zote anastahili kupewa Mungu kwa lo lote tufanyalo au kwa mafanikio yetu (Yer.9:23,24). Sasa tunamkuta mfalme Nebukadreza aliyekuwa ameuona uweza mkuu wa Mungu wa kuwaokoa wale vijana watatu katika tanuru ile ya moto, na kukiri kwamba "hakuna Mungu mwingine awezaye kuokoa namna hii" (Dan. 3:29), akijitukuza juu ya Mungu huyo kwa njia ya kiburi chake.
Mji wa Babeli ulikuwa na utukufu mkubwa sana (Isa. 13:19a).
Hakuna ufalme mwingine duniani unaoweza kuwa na utukufu kama ule. Mungu alimpa ndoto ya sanamu iliyowakilisha falme zote zitakazotawala kuanzia wakati wake mpaka Kristo atakapousimamisha ufalme wake (Danieli 2). Kwa kiburi akapinga mpango wa Mungu kwa kusimamisha sanamu ya dhahabu tupu (dhahabu iliwakilisha ufalme wa Babeli) katika uwanda wa Dura na kutaka watu waisujudie kama tulivyoona kwa somo la hapo nyuma . Kwa kiburi alimdharau Mungu wa mbinguni kuwa si kitu; bali kwamba yeye atadumu milele pamoja na ufalme wake. Aliishi na watu wa Mungu ili ajifunze juu ya Mungu wa Israeli; vijana wale wanne walikuwa fundisho kuu kwake. Hakujali yote hayo. Mungu katika upendo wake akamletea ndoto ya pili ili kumwonya aachane na kiburi chake sugu (Dan. 4:4-17).
Katika ndoto yake aliona mti mrefu uliokua mpaka mbinguni; wanadamu, wanyama, ndege wote walipata chakula chao katika mti huo. Kisha akamwona mlinzi mtakatifu akiamuru mti ule ukatwe kibaki kisiki tu kikapate umande wa mbinguni kwa nyakati (miaka) saba.
Kwa nini? "Kusudi walio hai wapate kujua ya kuwa Aliye juu anatawala katika ufalme wa wanadamu, naye humpa amtakaye, tena humtawaza juu yake aliye mnyonge" (Dan. 4:17). Ni wafalme wangapi wanaofahamu kuwa ni Mungu aliyewaweka katika viti vya enzi wanavyovikalia? hata leo tunapoona vitisho vya Vita baina ya mataifa ni kwa sababu wanasahau kwamba ni MUNGU aliyeruhusu wawe viongozi .
(Rum.13:1-7; 1 Tim. 2:1-6). Wajibu wa Serikali zote za dunia ni kusimamia utekelezaji wa Amri Sita za mwisho katika zile Kumi (Kut. 20:12-17).
Wanapofanya kazi yao hiyo vizuri na kwa uaminifu na haki mataifa yao yanabarikiwa. Wanapoingilia mambo yanayomhusu Mungu (Amri Nne za kwanza - Kut. 20:3-11) wanavuka mipaka ya madaraka aliyowapa na kustahili adhabu kutoka kwa Mungu.
Kumbuka kuwa Biblia sio kitabu cha siasa; lakini kuinuka na kuanguka kwa mataifa yote ya dunia kumeelezwa humo.
Ni Mungu anayetawala katika falme zote za wanadamu. Mungu anapima nyendo za mataifa yote duniani (Zab. 66:7-8; Zaburi 2; 9:17). Ni jambo la kusikitisha mno kwamba mataifa yote ya dunia, ukiwaondoa watakatifu waliomo, yataangamizwa vibaya siku ile ya mwisho kwa kwenda kinyume na madaraka aliyowapa Mungu.
je ,wewe hapo ulipo unatenda haki kama kiongozi ?.
(Ufu. 19:11-21). Danieli alipoitwa kuitafsiri ndoto ile ya mfalme "akashangaa kwa muda, na fikara zake zikamfadhaisha" (Dan. 4:19). Kwa nini alifadhaika?
Kwa sababu ndoto ile ilimaanisha kwamba mfalme angefukuzwa mbali na wanadamu na kula majani kama ng'ombe kwa miaka saba. Kwa nini iwe hivyo? Kwa sababu ya kiburi chake sugu. "Nyakati [miaka] saba zitapita juu yako; hata utakapojua ya kuwa Aliye juu ndiye anayemiliki katika ufalme wa wanadamu, naye humpa yeye amtakaye, awaye yote" (Dan. 4:25). Miezi 12 baadaye, "alikuwa akitembea ndani ya jumba la kifalme katika Babeli. Mfalme akanena, akasema, Mji huu sio Babeli mkubwa nilioujenga mimi, uwe kao langu la kifalme, kwa uwezo wa nguvu zangu, ili uwe utukufu wa enzi yangu?" (Dan. 4:29,30).
Unaona alivyokuwa anajisifu ? Pale pale tangazo likatolewa kutoka mbinguni kuwa ufalme wake umeondoka kwake na atakaa na wanyama akila majani kama ng'ombe kwa miaka saba mpaka atakapojifunza kumtambua Mungu wa mbinguni. Mafunzo ya miaka saba kukishusha kiburi sugu! Fikiria hilo! Mungu na ashukuriwe! Nebukadreza alijifunza kwa njia ya aibu sana (ya kuwa mwehu) kwa miaka saba mizima. Alitoka akiwa kiumbe kipya; akakitubia kiburi chake sugu na kuanzia hapo akaanza kumtukuza hadharani Mungu wa mbinguni (Dan. 4:34,35).
Ufalme wake akarudishiwa. Ushuhuda wake mbele za watu
ameutoa mwanzo wa Sura hii ya 4. "Mfalme Nebukadreza, kwa watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wanaokaa katika dunia yote; Amani iongezeke kwenu. Mimi nimeona vema kutangaza habari za ishara na maajabu, aliyonitendea Mungu aliye juu. Ishara zake ni kubwa kama nini! na maajabu yake yana uweza kama nini! ufalme wake ni ufalme wa milele; na mamlaka yake ni ya kizazi hata kizazi" (Dan. 4:1-3). Siku moja wale watakaookolewa watakutana na Nebukadreza mbinguni. Atawasimulia vizuri kisa chake.
Ni wangapi ambao Mungu anapozungumza nao katika Neno lake wanakaza shingo zao kwa kiburi na kuyatukuza mawazo yao juu ya Mungu na kufanya kinyume na maagizo yake? Je, wako tayari kupelekwa porini na kula majani ili wajifunze? Hilo ni zoezi kali mno. Je! Mungu atanivumilia mpaka lini asiukate mti wangu? (Luka 13:6-9). Yatupasa kutubu; la sivyo tutaangamizwa (Luka 13:1-5). Je, umewahi kufikilia juu ya kile ulichonacho unadhani ni nani aliyeruhisu ukipate ,je unamkumbuka Mungu kwa kukupatia usiseme ni kwaakiri zako maana pasipo yeye hatuwezi neno lolote.
Sisi si maarufu kuliko Mungu; wala sisi si bora kuliko wengine.hatuna haja ya kuwa wabishi pasipo sababu ,kuwa wenye viburi ,wasiotaka kubadirika mm Fredrick sylvanus ninaungana na wewe rafiki Mpendwa tushushe kiburi cha uzima tusisubiri kupata mapigo ndipo tujishushe ,leo nnakuarika Mpendwa ujitoe kwa YESU ndiye anayefundisha tabia njema ,ndiye anayetoa kiburi ,anarudisha na kuumba upya tabia njema ,Karibu umpokee YESU atakuweka huru Bwana akubariki ,
Karibu kwa somo linalofuata.
ConversionConversion EmoticonEmoticon